Jumatatu, 16 Januari 2017


KUFUNULIWA KWA KANISA LENYE MOYO MMOJA TU WA MUNGU

Wakili wa MUNGU Alianza ibada kwa uongoza wenye haki kutoa SADAKA YA: Kufuta agano la kutanguliwa kwa wenye HAKI Kila wanapotaka kushinda.
Ni sadaka ya kuishi ADEN na EDEN bila kutoka *kufika nimefika na kutoka sitoki*
Ni kusimamisha ukamilifu wa ushindi.
Kuingia EDEN na kukaa hapo hapo, baada ya kuondoa umbo la nyoka. Sasa tumefika kwenye ukamilifu wa ushindi.
Kuondoa agano la kutanguliwa kwa mwenye haki kila anapotaka kushinda. Katika kila eneo natangaza  ukamilifu wa ushindi kwa kuondoa agano la kutanguliwa.
Kanisa sio kwamba lilikuwa halija shinda, ukamilifu wa ushindi ulikuwa bado. Kila utakacho tamka ni lazima kitokee.
Leo tumepata ukamilifu wa ushindi, kazi ndio imeanza kwa mwenye haki kujiwekea ulinzi waovu wasikuvulie uchafu wao tena bali waokoke.
Mwa3:1-6, 3:1-3, moyo unaomwelekea MUNGU kwa kuongea sawa na Alichosema.
Mwa 3:4-6, moyo unaomwelekea kerubi kwa sababu ya kuamini uongo.
Hii ni mioyo miwili ndani ya mtu mmoja au ndani ya mwenye haki mmoja. Kuna kipindi unaongea kama MUNGU Alichosema, na kuna kipindi unaongea kama ndugu n.k nakuamini hata kama ni uongo.
SWALI: Ni kitu gani kilitokea hadi kerubi/ nyoka akafanikiwa kumdanganya mke wa Adam?
Mwa3:4-6, aliamini kuwa MUNGU nimbaya hataki tufanane naye.
Mkakati Katika Mwa3:4-6  nyoka alifanikiwa kuonyesha kwa mke wa Adam yaani kanisa kuwa MUNGU hampendi Adam, ila yeye kwa kuwa amewaibia  siri ndio mzuri.
MUNGU kuonekana mbaya, kerubi kuonekana mzuri.
Yale ambayo MUNGU Alikusudia kumpa Adam na mkewe hakupewa tena; Hiyo ndio hasara kwa kanisa. Hata vile alivyopewa Adam vilienda kwa kerubi.
Ndio maana mwenye haki kila anapofanya kizuri anaonekana kuwa anajipendekeza. Kila anachofanya mwenye haki kuonekana ni kibaya na mwovu kizuri.
MUNGU leo Anang’oa  kabisa huo moyo mwingine maana MUNGU Anataka moyo usio na mawazo wala makunyanzi.
Sasa moyo wa pili haupo tena na hauna nafasi tena ndani yako, ndani yako kuna moyo mmoja tu.
Moyo unaotokana na mataifa ulioenda, jamii, n.k haupo tena.
Sasa maongezeko yatakuwa makubwa maana kila kinacho toka hapa kinazaa matunda. Tumerudi katikati ya bustani ya EDEN hatutoki tena.
Ni wakati wa uzalishaji wa kumaanisha maana tumeingia CENTRE. Kile ambacho MUNGU Atakiachilia kwetu kitakaa hakitaibiwa tena. Kuna tabia ya kujihukumu kwa mwenye haki sasa tuache.
Nataka sasa umwambie MUNGU nitukanwe/ nisitukanwe kwenye kiini sitoki.
Yeyote akija kukuambia kinyume, mwambie kamwambie kerubi. Mimi sitoki.
+ufunuo 12:1-3 imefutwa kwa uhalisi.
+mwa1:2 Giza ukiwa na utupu mwisho.
+mwa2:8 mti wa ujuzi wa mema na mabaya umefutwa.
#kanisa tunakabidhiwa Mwa2:15 bustani kuilima na kuitunza.
Sasa MUNGU Anatuunganisha Na jeshi la:-
*kuwa na hakika ya safari kutimia.
*kuwa na hakika ya NENO kubarikiwa.
*kuwa na hakika ya kuinuliwa.
*kusudi la MUNGU kutokuzuiliwa na yeyote milele.
*aliyonena MUNGU yote yanatimia.
Ezekiel 36:26 MUNGU ametupa
#moyo MPYA.
#Roho mpya.
#Nafsi mpya.
Wakili amesema SILOAMU ambayo MUNGU alimpa Eliya Ad2 ndio imeanza Jana baada ya kufuta mioyo na tukabaki na Moyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni