Jumapili, 15 Januari 2017


KUOMBA AU KUSHUKURU KWA NAFSI YA MUNGU

WAKILI WA MUNGU alianza kwa kusema kila Neno litokalo Madhahuni ni lazima litokee. Neno la Madhabahuni ni lazima lithibitike.
1YOH 5:8 Umoja wa MUNGU, KRISTO NA KANISA = kila anae-kuona unaomba/unashukuru aone unashukuru kwa Nafsi ya MUNGU, Wote wajue kuwa sisi na MUNGU ni KITU KIMOJA.
Zab 27:4 kutafuta UZURI WA BWANA.
JE; unatafuta gari, nyumba n.k kwa ajili ya Nani? Kwa ajili yako ajisifie kwa wengine au kwa ajili ya utukufu wa MUNGU?
Kila mmoja leo ajipime hapa madhabahuni kama unataka kutubu/utubu kama kushukuru/ushukuru. Mdo 13:22-23 kwa kuwa unaomba kwa Nafsi ya MUNGU basi unampendeza MUNGU.
Unapo-nyoa leo hivi/kesho hivi ni kwa Nafsi ya Nani? =unapo-suka leo hivi/kesho hivi ni kwa Nafsi ya Nani? Unapo = weka hivi mara ukate hivi mara hivi ni kwa Nafsi ya Nani?
Wengi hatuna Moyo bali tuna-Mioyo na MUNGU anataka tuwe na Moyo Mmoja tu wa kwake Mwenyewe. MUNGU anataka sasa uombe kwa Nafsi yake sio yako.
*1samweli 11:1- ili hanna  apate mtoto ilibidi aombe kwa Nafsi ya MUNGU Waamuzi 14:1-3 Zab 50:12
MUNGU anataka Nafsi zetu tuziunganishe na yeye moja kwa moja, sio kwamba ana-shida. MUNGU anataka kila mahali ulipo aonekane lakini uwe na Moyo wake uombe kwa Nafsi yake.
Swali: nina Moyo wa kerubi ua wa MUNGU? Mwa 3:1-3
Ukiona unashindwa kuomba kwa Nafsi ya MUNGU ujue una- mioyo sio Moyo wa MUNGU.
Uwe na Moyo wa MUNGU mwenyewe ili ushukuru/uombe kwa  Nafsi ya MUNGU.
Tukubali kuanzia leo, tuwe na Moyo Mmoja Wa MUNGU ili tuombe kwa Nafsi ya MUNGU.
1 FALM E 3:5-13 kuomba kwa Nafsi ya MUNGU ni Chochote unachotaka kwa ajili ya utukufu wa MUNGU pokea sasa hivi. Unataka kibali, kutetewa  na uumbaji kwa ajili ya utukufu wa MUNGU pokea sasa hivi.
Je;unataka nini kwa ajili ya utukufu wa MUNGU? Pokea sasa hivi kila unachotaka
“kama unataka chochote kwa ajili ya  MUNGU apate heshima,utukufu,sifa; MUNGU ni lazima akupe”
Awali akijnga msingi wa ibada hiyo Wakili wa MUNGU alisema Zab 98:4- kila mmoja kumsifu BWANA -Furaha yako ni lazima ijulikane
“kila ambacho MUNGU amenitamkia ni lazima kitimie.
Ndani ya Moyo wa MUNGU cha kwanza ni sifa na sisi tunamsifu MUNGU, MUNGU hakuwahi kusifiwa”.
Ni lazima tumshukuru MUNGU kwa  kuwa tumependelewa mno, tumepewa Neema Kubwa.  Nataka nione furaha yako unapomwambia  MUNGU ASANTE.
Eze 34:1-23(a) MUNGU mwenyewe kuwaachisha kazi wachungaji wa kondoo na kutaka kondoo zake. MUNGU sasa anachunga kondoo  zake mwenyewe”. MUNGU kuweka Mchungaji Mmoja ambae ni YEYE MWENYEWE.
MUNGU amekuja mwenyewe maana anataka usiishiwe tena, usipungukiwe tena, usionewe tena, usilale njaa tena n.k.
MUNGU yuko na wewe hapo ulipo wewe utendae kwa HAKI, Hapohapo unapoanzia MUNGU anakuwa pamoja na wewe.
MUNGU ni Halisi kwetu formula zote za waovu kuangusha kanisa/Mwenye Haki zimefeli na hazipo tena. Adamu aliibiwa Nafsi Hai yenye Pumzi Hai na ndicho kinacho tafutwa na waovu kwa mwenye Haki.
Sasa MUNGU amekuja mwenyewe kuishi nasi hatoki wachafue /wasichafue hatoki.
SEMA;
Nidanganywe/nisidanganywe, nibezwe/nisibezwe/, nitukanwe/nisitukanwe n.k  EDENI NIMEINGIA SITOKI. Kama unajijua wewe ni Mwenye Haki basi yeyote anae kuja kushindana na wewe hashindani na wewe bali anashindana na MUNGU na huwezi kushindwa, tambua kila kitu chako kiko salama.
Aidha leo wenye haki wametoa Sadaka maalumu ya: “Kurejesha wema na ufahamu wa MUNGU mahali pake”
Kila aliyetenda Wema akiwa mwenye Haki, MUNGU alikuwa hatukuzwi na wewe mwenye Haki upewi hata asante. Kwa anzia sasa hivi, asifiwe na kutukuzwa MUNGU  kwa kila wema utendao.
Wema, Sifa, Utukufu  umerudi kwa mwenyewe na ijulikane kuwa Mfadhili  ni MUNGU sio yeyote.
Ukipanda Mema utavuna Mema, utatenda mema na kulipwa mema. mwovu hataweza kuchukuwa mema badala yako.
Toba kwa waliokuwa wanachukuwa wema,sifa, utukufu wa MUNGU.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni