Jumanne, 31 Januari 2017


*TUMETOKA MAUTINI TUMEINGIA UZIMANI.*                   
1YOH 3:13-14. Ndugu zangu tumetoka kwenye mauti tunangia uzimani.


Aidha SADAKA maalumu ya Leo niya kuondoa mauti kutuingiza uzimani.
Kufuta mauti yote ndani ya kanisa na kizazi cha MUNGU.
Ya kutoka kwenye mauti na kuingia uzimani.
Leo kanisa limetolewa mautini na kupelekwa uzimani.
Sisi tunajua ya kwamba tumepita toka mautini na kuingia uzimani.
Ni kituo kipya tumeingia kanisa cha kufutiwa mauti zote na sasa tumeingia ktk kituo cha uzimani.
Kituo hiki hakuna amchukiaye ndugu yake kwa kuwa amchukiaye ndugu yake ni muuaji.
Kituo tulichofika hakuna mauti MUNGU ametimiza NENO lake.
Agano la kichwa kanisa leo ni agano la Uzimani, ni la kutoka mautini kuingia uzimani.
Agano hili halitakaa lipate shida milele.
Agano hili limefutiwa kifo na mauti.
Agano hili limebarikiwa na MUNGU laana hazitakuwepo.
UFUNUO 20:6 huu ndio ufufuo wa kwanza sisi ni makuhani wa MUNGU na KRISTO wake.
Mahali hapa mauti ya pili haina nguvu tena.
KUNA TOFAUTI KATI YA MAUTI NA KIFO;
Mauti ya pili unatembea lakini vitu vyako vyote vimeibiwa/ vimekufa.
Kutembea ukiwa huna mikono kwa maana ya kila unachofanya kufa.
Huna akili ya MUNGU, ufahamu.
Huna agano la kichwa kanisa japo kuwa tunaona unaishi na kichwa wako na watoto unao lakini huna uzima.
Yaani hapo unatembea nafsi yako ikiwa kaburini ilishazikwa umebakiwa na roho tu ndio inadunda.
Lakini leo hatuna mauti tena maana tunatawala na kristo na tunamilikiwa na MUNGU mwenyewe.
MWANZO 2:17  walaikini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
MWANZO 3:6  akaona ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, wa utamanika kwa maarifa ….
Siku zote vitu vya kerubi huwa vinaushawishi urahisi wa wewe kuvipata lakini ndio unaangamia hivi hivi.
Unaibiwa nafsi yako kizembe , unauza thamani yako kwa vitu visivyokuwa na faida.
Vinakupa majuto makubwa mno ya muda mrefu, kitendo cha kuhiari kuwasikiliza walioshindwa waliofeli, walioasi, …. Tu!
Unaangamiza maisha yako yote, uzao wako ulionao na utakaokuja baada yako.
Unafuta yale yote ambayo MUNGU alikusudia kwako.
Leo umeingia kituo cha uzimani acha kusikiliza taarifa za wajinga.
Moyo mmoja wa kanisa umepokea na ndipo huo uzima unakaa.
Badilika geuka acha njia ambazo zinasababisha urudi nyuma.
MUNGU anapowaadhibu waliokuwa wanakutesa usiwaonee huruma maana yeye MUNGU amekusamehe, amekutakasa, amekuvika vazi jeupe, amekugharamia kwa ajili yake yeye mwenyewe.
Achilia sahau ili MUNGU aingie kazini mwenyewe wewe mwenyewe huwezi kujitetea na huwezi kupata haki yako.
MWANZO 5:3 Kuuza mtoto wa kufanana naye badala ya mtoto wa kufanana na MUNGU.
Je hujawahi kuona mtu anaumwa mpaka anaanza kuoza ile ni mauti ina maana huyo mgonjwa mauti ilishamvaa kinachosubiriwa hapo ni kifo japo anaongea.
Hayo yote ni kwa sababu ya kutokuwa na utii katika yale ambayo MUNGU alisema nao wakashindwa kuwa na umoja wa MUNGU.
Ubinafsi ndio ambao ulisababisha kuzaa wa kufanana nae badala ya kufanana na MUNGU.
Kutokuwa na moyo wa toba na unyenyekevu, kuwasukumia wengine mabaya badala ya kutubu.
Leo tunaishi na tunatembea na MUNGU hivyo mauti ya pili haipo ndani ya agano, biashara, kazi, familia, pia kila utakachoanzisha kitaleta faida.
Kizazi hiki cha MUNGU KRISTO NA KANISA hakuna mauti milele.
1KOR 15:20-28 sharti amiliki yeye aliyevitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.
Adui wa mwisho aliyebatlishwa ni mauti, hatutaishiwa maana hatuna mauti. Limbuko ni kristo na msingi uwe ni kristo, maana mwisho naye tumeupata.
MUNGU amesema hatoki kwetu lakini hawezi kukaa mahali penye mauti.MUNGU hawezi kutawala na aliyevikwa vazi la mauti.
KRISTO kz4 alisema iko majira inayokuja ambayo MUNGU mwenyewe atakuja.
Kwenye dini hawakufundisha kwamba MUNGU atakuja ila walitufundisha kwamba yesu atakuja.
Sasa MUNGU amekuja mwenyewe na mwana amemtiisha chini ya miguu yake ili MUNGU awe yote katika yote.
EFESO 1:9-10  Atajumlisha vitu vyote vilivyo mbinguni na vilivyo duniani view vya kwake.
Hii ni majira ambayo MUNGU hakai mbinguni tu bali anakaa katika nchi, anatembea katika nchi, anatawala katika nchi.
MUNGU amekuja kumiliki.
MATHAYO 21:33-43  Amekuja kuangamiza vibaya wabaya wote.
Taifa lenye kuzaa matunda limepatikana, ni taifa la Gosheni ambalo ufalme wa MUNGU.
YOHANA 19:1-18  Ukiona agano /ndoa yako ina migogoro ujue kwamba mauti imeingia.
Yesu alivikwa vazi la mauti, zambarau.
Wakaanza kumpiga mateso kutemewa mate nk ukiwa na vazi la mauti huwezi kupata haki yako.
Pamoja na kuwa hujatenda dhambi ulikuwa unauawa kwa sababu una vazi la mauti.
Mwenye haki hata kama hana kosa alikuwa anasingiziwa uongo ili mradi tu achukiwe afukuzwe kazi
Kwa kuwa mauti imefutwa hakutakuwa na mateso milele.
Pilato hakuona kosa kwa Yesu lakini alishindwa kumsaidia kwa kuwa alikuwa amevikwa vazi la mauti.
Tunamshukuru  MUNGU kwa kuwa sasa kweli imesimama, pilato nae anajua kweli na mwenye haki hataonewa tena.
YOHANA 18:37 kizazi kile pilato hakuijua kweli,alikuwa ni mkubwa serikalini lakini hakujua kweli.
Ndio maana tumetoka mautini na tumeingia uzimani kwa kuwa kweli imesimama.
Wote walikuwa ndani ya kizazi cha MUNGU, vazi la mauti limeondolewa kwao.
LUKA 1:45  Heri aliyesadiki haya yote aliyoambiwa na BWANA maana yatatimizwa kwake yote aliyoambiwa na BWANA.
Unaweza kujiuliza kwa nini tunavaa pete mkono wa kuume ZABURI 45:6
Mabinti wa wafalme wapo pamoja na wameketi mkono wa kuume.
MWANZO 48:1-  Efraimu alikuwa mdogo lakini alikuwa au aliwekwa mkono wa kuume, wakati wa kubarikiwa kwake.
Efraimu maana yake kanisa.
MHUBIRI 10:2 MOYO WA MWENYE HEKIMA UPO MKONO WA KUUME.
Lakini moyo wa mpumbavu upo mkono wa kushoto.
Kanisa tunawavika mabibi harusi pete mkono wa kuume kwa kuwa twajua tufanyacho.
Yusufu alipoona Efraimu amewekwa mkono wa kuume na ni mdogo, Yusufu alisema sio hivyo baba baba yangu…. Israeli akasema nyamaza kimya najua mimi najua.
Kuanzia leo umepokea kuishi uzimani siku zote, usisikilize sauti yoyote kinyume na NENO linatoka madhabahuni.
Tumepokea agano la kutembea na kuishi  na MUNGU uzimani.

Jumatatu, 30 Januari 2017


KUFUNULIWA KWA MOYO MMOJA PEKE YAKE KWA UHALISI

Nanyi mtakuwa wa MUNGU na MUNGU ni wangu/wako milele. EZEKIEL 36:26
Ni mahali tumefika  pa kuogopwa na kila kitu, waganga, wachawi, walozi, magonjwa umasikini ufukara kuishiwa  nk kwa kuwa tumekuwa wake MUNGU.
MAJIRA HII; Yeyote akija kwa hila utajua tu, atakayekubariki utajua tu kuwa Baraka hii ni ya namna gani, atakayekuja kwako utajua tu ujio huu ni wa aina gani!
WAEBRANIA 8:10-   MUNGU amesema kuwa atatutoa uchafu wetu kwa maana atafuta dhambi zetu na kutusafisha.
Mahali tulipofika hatasimama muovu wa aina yoyote.
Ndio maana anasema kuwa ataziandika sheria zake ndani ya moyo wangu/wako.
Sasa ni ile majira ya aliyemdogo na mkubwa kumjua MUNGU.
Aidha Sadaka Maalumu iliyosimamishwa leo ni kufunuliwa kwa Moyo mmoja peke yake kwa uhalisi.
Sheria ya MUNGU ikiandikwa ndani yangu /yako utajua tu kila kitu kilichoko mbele yako.
Sheria ya MUNGU ikiandikwa ndani yaa moyo wangu/wako MUNGU anaita utajiri uje kwangu na kuuongeza mbele.
Ni majira ya kuita karamu ije inakuja na maongezeko pia.
MUNGU atazidisha matunda ya mti na mazao ili usipatwe na njaa.
Atakuongeza ili usitukanwe kwa ajili ya njaa, maana tumefika mahali ambapo hatutukanwi tena wenye haki.
Kama walikuwa wanakuita tasa kuanzia leo wewe sio tasa tena milele, uliitwa masikini kuanzia leo wewe ni tajiri hutaitwa maskini tena.
Ni majira ya wewe mwenyewe kuichukia dhambi, hutatenda dhambi kwa amani milele.
NENO linasema amani haipo na haitakuwepo wa waovu watenda dhambi milele.
MUNGU atanitajirisha kwa ajili yake yeye mwenyewe.
Atakusafisha, atakutoa uchafu, ili uwe safi kwa ajili yake yeye mwenyewe.
MUNGU atanigharamikia kwa ajili yake yeye mwenyewe ili nifanane nae.
WAKILI wa MUNGU alimnunulia mavazi 7 mtendaji wake ili afanane nae.
WAKILI WA MUNGU alimvika vazi Mtendaji wake ili afanane  na yeye ili pia ukimuona Mtendaji ujue umemuona WAKILI WA MUNGU.
Hivyo MUNGU atanitengeneza vizuri kwa ajili yake yeye mwenyewe, atatengeneza agano lako, familia yako biashara yako kazi yako kwa ajili yake yeye mwenyewe.
Kwa hiyo itakuwa kwa kila anionaye atamuona MUNGU KRISTO NA WAKILI WA MUNGU ndani yangu.
Kila nitakapoenda watauona ule utatu wa MUNGU.
MUNGU hapendi kuitwa mchafu  ndio sababu analazimika kunisafisha kunitakasa kuondoa mavi walioninyea, mikojo walionikojolea, walivyoniharishia kwa ajili yake yeye mwenyewe.
Siku ile nitakapoitakasa …. Palipobomolewa…. MUNGU atapafanya kuwa pazuri.
Mahali pa mateso kudhulumiwa kudharauliwa kutukanwa MUNGU amepafuta ili niwe safi.
MUNGU anafanya haya yote kwa sababu majira zote 6 hakuwahi kuabudiwa wala hakuwahi kupata wa kumuabudu yeye katika roho na kweli.
*IBADA YA KUMTOA BINTI/KIJANA KIUNGU.*
Kwa nini tunamtoa binti na kijana kiungu?
Je ni lazima kumtoa binti na kijana kiungu??
Msingi wa ibada hii ni kile alichosema mwenyewe.
MWANZO 2:24 Mafanikio yako yapo katika kile MUNGU aliongea nasi alisema nasi alichoagana nasi,
Ukiwa nje ya kile alichosema MUNGU huwezi kukutana na mafanikio yako.
Lakini pia lazima ujiulize ya kwamba Je unaanzaje kwenye agano lako?
ZABURI 11:3 msingi ukiharibika mwenye haki atafanya nini? Mwanzo wa familia ukiharibika utafanya nini?
Msingi ndio unaoamua hiyo nyumba idumu kwa muda gani! Au hiyo nyumba iwe gorofa au ya ukubwa gani!
Maana msingi wa vyumba viwili huwezi kujenga gorofa ni mpaka uwe umejenga msingi wa gorofa.
Binti kijana anaposhindwa kutoa kwa wazazi ndipo tatizo linapoanzia, ndipo shida inapoanzia na ndipo taabu inapokuwepo.
Maana unakuta wameoana lakini wote wawili mioyo yao ipo kwa wazazi, moyo wa binti uko kwa baba na moyo wa kijana uko kwa mama.
Wewe ukikuta baba anayesema nitakurudisha kwenu ujue ni Yule ambaye moyo wa agano aliuacha kwa wazazi.
Hivyo hajui kwamba hata wewe kanisa wake ulitoka kwenye ubavu wake.
Akisema urudi umwambie kwetu ni kwenye ubavu wako, nawezaje kuwa na kwetu zaidi ya kwenye ubavu wako kichwa wangu.
utoke mahali pa uvulana na usichana; mpaka sasa kuna wazazi ambao bado wana usichana na uvulana.
Siku zote asiyependa kupika ujue huyo bado ana usichana anaona bora aende kibandani akanunue chipsi kupika aa!
Ukiwa mvulana pia unaweza kuondoka na kwenda popote bila kuaga.
Uvulana kupenda kula chakula cha gengeni, kuliko urudi ukale mlima wa moto kwa kanisa wako unasema aaa ngoja nikale kwa mama nitilie.
Usichana ukienda kwa rafiki yako ukiona muda umeenda unasema mimi nalala huku huku hata aibu huna umemuacha kichwa wako apumzike peke yake.
Kuna wababa ambao hata wakifuliwa mavazi wanakuja kurudia kufua kanisa akipiga pasi anakuja kurudia kupiga pasi huu ni uvulana kutomwamini kanisa wako.
1KOR 3:9 MUNGU kupitia Paulo alisema wa kila mmoja na aangalie jinsi anavyojenga huo msingi  ni msingi gani unajenga?
MUNGU amesema kuwa kijana anatakiwa atoke kwa wazazi wao  ataambatana na binti hao watakuwa si wawili tena bali ni mmoja 1+1=1.
HESABU YA MUNGU                                                                                                                NI 1+1=1
Hapa ndipo MUNGU alipowapiga chega wana mahesabu ya dunia na ulimwengu, sayansi, tenolojia.
Leo kijana na binti wanatoka kwa wazazi wao.
Pia wanatoka kwenye uvulana na kwenye usichana.
HESABU 30:1-  Kuna nadhiri ya binti kwa babaye, leo tunavunja ule uhusiano wa baba na binti ili binti akimuona kichwa amuone na baba yake huko.
Vile vile kijana anatakiwa akimuona kanisa aone amemuona mama yake, shida zote alizokuwa anampelekea mama yake akuletee wewe kanisa.
Na wa mama muwaachie vijana wenu musianze kusema ooh!!
Nilikuweka tumboni miezi 9 hapana kwa upendo wa MUNGU ili wawe na mafanikio mazuri mama baba muwaachilie vijana wenu.
Ulikuwa na swali muulize kichwa wako, muulize kanisa wakona vilevile wewe kanisa kichwa unapoletewa swali umjibu mwenzako vizuri kabisa.
Acha kusambaza maneno ya familia yako agano lako.
MITHALI 31:10- Kilichomponza hawa ni kwa sababu ya kuwa na kinywa chepesi kujibu ujuaji mwingi akajikuta anajibu hata maswali ambayo japo anajua lakini ilikuwa sio haki yake kujibu.
Kanisa mwema hakai kwenye nafasi ya kichwa wake.
Ukikuta mama anayekaa kwenye nafasi ya kichwa wake mwangalie vizuri utakuta hata agano familia yake haipo vizuri.
Agano linakuwa na mafarakano muda wote, watoto na wazazi hawaelewani muda wote.
Ukikuta kichwa kavaa vibaya shida ni kanisa, kichwa kanisa unatakiwa kuuweka wazi mwenzio.
Kanisa unatakiwa kuamka mapema kabla usiku haujaisha, usikubali kichwa aende kazini bila kunywa mtamu tamu.
Uongee kwa hekima, acha umbeya, maneno maneno.
Usiwe msemaji zaidi kuna wakati unatakiwa useme hili naomba ajibu kichwa wangu.
ISAYA 6:9 ufalme upo mabegani mwake, vichwa ni wafalme.
Ukijifanya mkali unasababisha na baba awe mkali bila sababu.
Jifunze kukaa kimya, acha baba aseme kwanza. Kanisa isifike mahali ukawa muamuzi wewe.

Jumapili, 29 Januari 2017

MOYO NI NINI?

WAKILI wa MUNGU kabla ya kufundisha NENO la leo alikuja na; -
Zawadi ambayo jana alituahidi. Akasema anafuraha mno, na furaha yake ya kwanza ni kwa sababu  kwa mara ya kwanza ameona gari lililoandikwa “waliookoka wana raha”.
Kwa sababu hiyo sitakiwi kuona mateso, magonjwa, hasara, giza ukiwa utupu, nk kwa sababu umetoka ukoo Fulani.
Mshale wowote uliowahi kukutana nao kwa sababu ya asili mahali ulikotokea, ile nguvu ya umbo ya kukuingizia majuto, kujihukumu, matatizo, shida.
Hata kama umepigwa na kukanyagwa sana leo sahau kabisa, ulivyotukanwa, ulivyobezwa, leo samehe na usahau kabisa.
Furaha ya pili Ezekiel 28:18 Alipoinua moyo wake automatically moto ulitokeza ndani yake mpaka akawa majivu.
Hivyo leo chochote kilichoinuka kinyume na mimi leo au majira yoyote moto umetokeza ndani yake na umemteketeza kila aliyenidhulumu, aliyenisema mabaya.
Waliokuwa wanatesa agano lako, biashara zako, familia, kazi yako leo moto umetokeza ndani yao. Kwa Yule kahaba aliyechukua kichwa wako, chuma ulete kwenye biashara zako moto umetokeza ndani yake na umeteketeza.
Aliyenifanyia hila, aliyekuwa anazuia kiwanda changu, mashamba yangu, leo moto umetokeza ndani yake na amekuwa majivu, najisi, kitu kisichofaa.
Na wale wanaoenda kwa mganga kutafuta msaada na mganga mwenyewe moto umetokeza.
Wanaoenda kuzimu kujificha moto umetokeza ndani yao.
Waliokuwa wanaisema SILOAMU vibaya leo moto umetokeza ndani yao.
Wale waliokuwa wanawatesa wenye haki, waliochukua vitu vyako leo moto umetokeza kwao.
NENO hili kama halikutokea kwa kerubi haitatokea kwako lakini kama ilitokea kwa kerubi sawa na MUNGU alivyosema basi hata kwangu leo lazima itokee.
Vikao walivyokuwa wanafanya vya kuangamiza kanisa leo moto umetokeza kwao.
Ulikuja kwa nauli ya kukopa leo kwa ibada hii ukitoka hapa lazima upokee simu ya kwamba kila kitu kimetiki.
MUNGU amelifuta umbo la zamani  hivyo sitakumbuka mambo ya kale ya zamani milele, ramani kundi la waovu michoro yote waliokuchorea ya kuangamizwa , kukupiga wewe mwenye haki leo moto umetokeza kwao.
Isaya 43:18  
LEO lazima utoke na jambo jipya . KIAPO; LEO UNAONDOKA HAPA NA JAMBO JIPYA.
Tena ukiwa ni amwingine kabisa, mpaka sura yangu itabadilika, nitaonekana kwa kila anionae ataona mwanga mionzi ya utukufu.
Yule malaika anayefuta mateso yote kwa wenye haki yuko hapa, Jeshi linalofuta kumbukumbu mbaya  zote liko hapa.
WAKILI WA MUNGU; ametaka baada ya ibada hii, baada ya kusoma ibada hii, baada ya kusikiliza ibada hii kila mmoja amuone amekuwa na muonekano sura kama ya mtoto.
ILI KUTOKA KABISA KWENYE UMBO LA MTU NA MWANADAMU;  kwenye mateso yote tumetoka, kwenye kumbukumbu mbaya zote tumetoka. 
Leo sahau kabisa kwa wewe ambaye unajiona umetoka kwenye familia ya umasikini, leo nataka uone ya kuwa wewe ni mtoto wa mfalme.
Kujiona umetoka mabonde kwinama;
Kuanzia leo wewe mwenye haki  lugha yako ibadilike, muonekano wako ubadilike, aliyewahi  kuzaliwa katika shida na akaitwa shida leo asahau shida zote.
Sahau ili yote ambayo MUNGU ameyaandaa kwa ajili yako leo upokee. Maana pasipo kusamehe na kusahau huwezi kupokea.
Kama bado nakumbuka ya zamani leo nisahau ili nivuke na nivushe familia, kijiji ulichotoka.
Leo tunafuta kabisa umbo la mahali ulipozaliwa, hata kama ulizaliwa na chifu ujue leo MUNGU ndio chifu, ama na mfalme jua leo MUNGU ndiye mfalme.
Na leo MUNGU amenitoa kuwa wa mwisho na sasa leo mimi ni wa kwanza ambaye napewa fimbo ya chuma.
Kuna wanaokumbuka mpaka leo yaliyotokea kule shule alikosomea jinsi mwalimu alivyompiga kwa kosa la kuonewa, anakumbuka rafiki yake alivyomuibia akili yake nae akafelishwa.
Daniel 1:3-8 ulikuwa ni kijana mzuri tu ghafla unakutana na wakaldayo ambao walikufundisha tabia mbaya unakunywa pombe, unavuta sigara bangi, kuzini, kuiba, kuwa na hofu mashaka wasiwasi leo samehe na usahau.
Yote uliyowahi kukutana nayo ukiwa shuleni leo usahau.
Leo MUNGU ananipa moyo mwingine moyo mpya moyo mmoja kabisa  nachotakiwa ni kuondoa kumbukumbu mbaya zote.
Danieli anasema hata jitia unajisi kwa chakula cha mfalme, hata wewe muapie MUNGU weka agano nae kwamba hutajitia unajisi kwa chochote kinachotaka kukutoa kwa ALIYETUMA WOTE VIZAZI VYOTE.
Kama Daniel alishinda na mimi leo nimeshinda. Usiseme haiwezekani inawezekana vizuri.
Kuna waliowahi kunajisiwa na ndugu yake kabisa, ni kaka baba yake aliwahi kumbaka leo samehe  na uachilie na usahau kabisa maana ni wakati wa kuwa matajiri tena kwa uhalisi.
Ujue rohoni kuna mapepo mengi yanayozuia wewe mafanikio yako.
LEO NAPOKEA BRAND NEW HEART
Kuna walioonewa kazini wakafukuzwa, wakafungwa, wakahukumiwa, wakatuhumiwa nk samehe na usahau, uone MUNGU atakavyokufanyia promotion MWANZO 39:1- yusufu alionewa lakini MUNGU alimuinua kwa majira  husika ilipofika na hakuyaweka moyoni.
Yusufu hakushitaki hata kwa baba yake jinsi ndugu zake walivyokuwa wanamfanyia  kwa sababu alijitambua kwa ile kanzu ambayo baba yake alimshonea alijua kuwa yeye ni wa tofauti.
Leo MUNGU amekushonea vazi jeupe vazi la utakatifu vazi la uaminifu na uadilifu  lenye kukutofautisha na kutangaza ndani ya uumbaji wote ya kuwa umetoka kwenye dhiki kuu.
Yusufu aliijua hatma yake na wewe mwenye haki leo tambua kuwa hatma yangu haikuwahi kuguswa na yeyote ila tu MUNGU anataka nisamehe na nisahau ili itokee.
Kuna wanaokanyagwakanyagwa kwa sababu kuzuia rushwa, hata kama ndugu zako ukoo wako ndiyo wamekunenea maneno mabaya ya kukulaani leo nataka usamehe na usahau.
Maana kuanzia sasa watakutafuta watakuja huku wamepiga magoti maana watajua kabisa kuwa kweli ni ipi maana kweli imepata mahali pa kukaa hivyo watajua kuwa huna kosa.
Naona kama mnashangaa sana hamuamini kama iatokea??? Je Yusufu hakufuatwa gerezani??
Kuna aliyedhulumiwa mshahara wake leo unarejea.
Kila aliyewahi kuchukua marupurupu yako leo amerejesha.
IT IS PAY BACK TIME
Kuna walioteswa kwenye agano huko walikoolewa mpaka wanajuta wanaona kama walikosea jinsi mawifi wanavyomtesa, mama mkwe nk leo samehe na sahau.
MUNGU amewakumbuka leo unachotakiwa kufanya mama sahau yote, baba sahau yote. WAAMUZI 14: Samsoni na delila.
Kuna mabinti wamechumbiwa, kuna vichwa wamechumbia halafu wakaachwa bila sababu tena hawukuambiwa taarifa yoyote.
Binti kijana tambua leo MUNGU amekuandalia bonge la kichwa /kanisa kwa ajili yako, leo wewe samehe na sahau.
Kuna walioibiwa na kudhulumiwa fedha zao, nyumba zao, mashamba yao, viwanda vyao nk 1FALME 21:1-  Wenye haki walipata shida mno majira hii MUNGU hakubali milele.
Leo usamehe na usahau maana kuna mkong’oto unaoendelea huko lazima watakuja huku wanakimbizana kukutafuta ili wakulipe haki yako.
Kujipigania wewe mwenyewe haiwezekani unatakiwa umuachie MUNGU ALIYETUMA WOTE kwa wewe kusamehe na kusahau ili MUNGU atende mwenyewe apendavyo kumtenda muovu LUKA 19:27.
Kuna walioonewa kwenye dini, dhehebu na wengine wameonewa humuhumu ndani SILOAMU leo nataka uwasamehe na usahau.
Maana kwa yaliyotokea mpaka wengine wanaota mpaka kwenye ndoto.
samehe Sahau ili uone MUNGU anavyofanya maana zile kamba zilizokuwa zimemfunga zinafunguka sasa hivi.
Wote niliokuwa nimewarundika kwenye akili ya kushoto na kulia, wakanielemea mpaka kuimba nikawa naimba flati  kwa kuwa akili ya kushoto imebeba sauti nzuri, ufahamu mzuri akiba njema, akili ya kulia imebeba mahesabu makali.
Sasa ili nijue kweli umesamehe na kuachilia na umesahau ntaona tu jinsi unavyoimba, producer  ukipiga gitaa hiyo ndio nitajua kama umesamehe na kusahau. Ukikuta mahali wanaimba vibaya, flati ujue kuwa akili ya kushoto imeelemewa.
Akili ya kushoto ikielemewa  oooh!!! Utasikia flat tu!
Kuna waliomlaumu MUNGU AYUBU32:1- Usimpe orodha MUNGU ya vitu ulivyofanya kwa madhumuni ya kuhesabiwa haki.
Usimwambie MUNGU ujue mimi ndiye natoa sana hapa madhabahuni, nilimsaidia na kuhani … kulipa kodi ya nyumba ujue bila mimi angefukuzwa.
Leo tambua ukitoa sadaka ikakubaliwa umshukuru mno MUNGU, kuhesabu uliowahi kuwasaidia ni sawa na kujihesabia haki machoni pako mwenyewe.
1SAMWEL 15:20- MUNGU ALIYETUMA WOTE anapenda utii kuliko……… anachokuambia ufanye amesema sahau samehe ili awaangamize leo adui zako fanya hivyo ona hivyo na ishi hivyo.
WAKILI ; amesema yeyote haruhusiwi kujivuna, maana hata yeye haruhusiwi kujivuna wala kuringa, yeyote asiringe kuanzia  MIAKA 1000 mpaka wa kwanza sana.
Aidha katka ibada hii Wakili wa MUNGU amefunua Jeshi Maalumu na Moto maalumu wla kuhukumu na kuteketeza kabisa akiba mbaya zote ndani ya Moyo wa kila mwenye Haki yetu.
Hivyo leo tunafuta kujihesabia haki tunataka wewe MUNGU ndio utuhesabie haki.
Sadaka maalumu ya leo Yeremia 30:23-24 ghadhabu ya MUNGU. Isaya34:8 kisasi cha MUNGU, 1PETRO 1:17 kiti cha MUNGU kuhukumu.
Alisema sadaka maalumu ya leo inahukumu uovu wote tangu mlimani maana Wakili alitubu kwaajili ya uovu wote tangu mlimani na vizazi vyote. 
Wimbo; Sitatoka kama nilivyokuja nimekutana na BABA…….. KRISTO…….. WAKILI WAKE……. mahali hapa yupo MUNGU ( ALIYETUMA WOTE VIZAZI VYOTE.
MUNGU tayari yuko hapa na sadaka hii imepata kibali mbele za MUNGU.
Kila aina ya kichaka cha mateso taabu nk kinaungulia hapa kwenye sadaka.
Kwa sadaka na shuhuda sitakutana na mateso tena MUNGU yuko hapa kuhukumu yote.
Hata ule mwiba MUNGU ameuondoa. Sitakumbuka mabaya tena maana moto umetokeza kwao.

Nashukuru kwa ajili ya waimbaji  wamesema kweli inakaa ndani ya moyo. Pale MUNGU alipoanzia ndio tumefika, ndio sababu MUNGU ametupa leo somo la MOYO.
Mawazo , kumbukumbu, ujuzi, ufahamu, kufikiri  yaliyokuwa ndani ya moyo.
Katika mengi zaidi kulikuwa na mioyo mingi badala ya moyo mmoja.
Kwa nini moyo umechorwa hivi  kwenye zawadi tuliyopewa leo tofauti na jinsi ambavyo tumezoea, tofauti na ambavyo huwa unachora na tofauti na ulivyofundishwa shuleni.
Moyo ni nini ? ZABURI 19:14 Uone ndani ya moyo jinsi ambavyo kunakuwa na mawazo mengi tena tofauti tofauti.
Yaani umekaa ibadani sasa hivi lakini unasababisha uende  pishoni, mlima wa moto , ofisini, nk ukiwa umekaa hapohapo.
Daudi aliwaza na kwa majira ile ilikuwa ni lazima uwaze na ilikuwa inaruhusiwa, hivyo aliomba kwa MUNGU kwamba mawazo yake yapate kibali.
Majira hii haturuhusiwi kuwaza bali ni majira ya TENDO MOJA HALISI. Kwa hiyo unaomba upate kibali kwa tendo.
Usiposalimiwa tu unawaza kuwa anakuchukia wala huwazi kwamba atakuwa ameamka ana mawazo mengi aa huwazi kuwa huko alikotoka kakutana na mangapi!
Ukiona wanaoongea mpaka wanagonga tayari umeshawaza wanakusema wewe.
Kuanzia leo miaka yote 1000 ya kutawala na KRISTO sitakuwa na WAZO BAYA milele.
LUKA2:19 Lakini Yule mariamu aliyaweka yale maneno moyoni mwake.
Moyo huwa unafikiri tatizo ulikuwa siku zote unafikiri mabaya.
Hata WAKILI hizi siku 3, 4 ambazo hakuonekana kuna waliofikiri sijui amenuna, amekasirika amezira wala hakuna aliyekuwa anasema atakuwa ameenda vituo vingine, au atakuwa ameambiwa na MUNGU abaki.
Kuna wengine walipewa taarifa za uongo na waliofeli tangu lini waovu wakaijua  sauti ya mchungaji mmoja? Kuanzia leo mimi….. sitaisikiliza taarifa za waovu nikaziweka ndani ya moyo zikaniumiza.
Sitakutana na taarifa ya mjinga nikakubali nikaweka ndani ya moyo.
Leo naondoka na moyo wa MUNGU ALIYETUMA WOTE VIZAZI VYOTE unaoona mema tu!
Jinsi moyo ulivyokuwa na mambo vitu vya hovyo!! KUMB 8:5
WAKILI alisema “mara nyingi nikimkemea yeyote hapa wengi huwa mnawaza  mnafikiri kuwa kuna kitu nimeambiwa nimesikia kwa yeyote”.
Bali leo tambua kwamba sio kweli kwamba anakuwa ameambiwa bali ni MUNGU mwenyewe …. Kuna Neno linasema BABA humrudi mwanae…
MUNGU ametupa mwanzo malidadi tunatakiwa tuwe na moyo mmoja wa MUNGU usiosikiliza taarifa maneno, mambo mabaya yote nk
LUKA 6:45  tabia ya leo unanena mazuri kesho mabaya imefutwa na wengi tumekutana na watu wa aina hiyo, leo unaelewana na kichwa/kanisa kesho ngumi hamuelewani tena, leo unaelewana na watoto, majirani, ndugu kesho hamuelewani imefutwa.
Leo MUNGU anayaondoa yote maana ni wakati wa kuja na fungu la MUNGU yaani fungu la kumi kikapu imejaa .
Kwa hiyo leo hicho chumba na nafasi ndani ya moyo kimefutwa , leo vyumba viwili vimeondolewa kimebaki chumba  kimoja cha HAZINA NJEMA.
MOYO WA KANISA ninaosema mimi ni ule moyo ulioungana na nafsi sio ule moyo unaokaa upande wa kushoto ambao unakuwa na pande mbili na unachorwa na mkuki.
ZABURI 119:11-   ZABURI 27:4    Ifike mahali ujuzi wako uwe ni NENO tu! Ufahamu wako uwe ni wa NENO, kumbukumbu na mawazo na kufikiri kwako iwe ni NENO pekee.
Unafahamu kwa nini dar-es-salaam iliitwa bongo?? Ni kwa sababu ya uongo, udanganyifu hivyo ikatokea bongo fleva sifa za uongo, zilianzia hapo.
Ndio sababu mtoto akiwekewa bongo fleva hata kama upo kwenye daladala tu utaona anacheza.
kijana ukiweka bongo fleva anacheza utasema aliwahi kwenda disco kumbe ndio kwa mara ya kwanza anaisikia ndio utaona anavyojinyonga nyonga kama nyoka.
Kwa kweli leo tumepona kabisa kabisa! Maana MUNGU asingenipa huu moyo wake sijui ingekuwaje.
Kwenye mtihani wowote utakaokutana nao leo utajua tu cha kujibu maana umepewa moyo mmoja wa MUNGU na umejaa NENO.
Leo naondoke na moyo mpya ule wa zamani nauacha leo madhabahuni uungue kabisa.
MITHALI 3:3-4 Rehema na kweli zisifarakane na mimi mwenye haki milele.  Yaani kusamehe bila kuombwa msamaha.
Ndio sababu nilikuambia ninapoona yeyote anataka kunikosesha namuona kama kichaa kwangu.
Mimi siishi kwa nafsi yangu wala kwa ajili ya family yangu bali naishi kwa ajili ya kizazi cha MUNGU.
Unafikiri MUNGU anapothubutu kuapa kuweka agano au kusema kwa kutumia kinywa changu na kusema kuwa   Tanzania ni urithi wake unafikiri mimi natakiwa kukaakaa tu?
Lazima kila siku niombee taifa  hata kama kuna polisi na wana silaha lazima niombee TAIFA. Niombee viongozi wote.
Mimi huwa sina tabia ya kuja kukuuliza eti nimesikia umesema hivi. Acha kuuliza utafuta kujitetea je utawafuata wangapi?
WAKILI WA MUNGU; Leo ujue kama ulikuwa unafikiri unajua mimi ni mtu leo ujue kuwa mimi sina chembechembe za mtu wala mwanadamu.
Ndio maana sina kikao na yeyote.
Kama wewe unataka moyo huo chukua , usimhukumu yeyote kwa maneno ya kuambiwa, usimshitaki yeyote.
Usimhukumu RAIS maana kuna wengine wanamhukumu tena kwa maneno ya kusikia.
Wengine mnathubutu kunihukumu hata mimi WAKILI WA MUNGU hamjui mtakufa? Je mlijua ELIYA AD2 anadanganya?
Maana Eliya alinitambulisha mimi kwenu, Akasema afadhali mnikosee mimi mtasamehewa lakini msimkosee MIAKA 1000 kwa kuwa hamtasamehewa milele na MUNGU.
Sasa je hao wanaonitukana wananishitaki je mnafikiri MUNGU atawaacha? Hawezi kuwaacha kabisa!!
Je hawakumjua ELIYA? Je hawakusikia? Je hawakuwepo hawakuonywa hawakuambiwa? Je hawakumwamini? Je hawajaishi nae?
Leo naondoka na moyo usiokufa, usiougua, usiolazwa mwananyamala, usiopungukiwa, usioishiwa, usiokutana na huzuni uchungu mateso usioona kutukanwa, usiozimia usioanguka Isaya 40:28-31.
NAONDOKA NA MOYO USIOISHIWA KILA SIKU SHANGWE NA NDEREMO.
Je huu moyo unaupenda? Uchukue huo! Moyo usioshitakiwa mahakama yeyote, haufungwi hauingizwi selo.
Kama mlijua mimi ni mtu, mimi sio mtu, nasema sio mtu mimi Wakili amesema.
NJIA ZA BWANA waambie kweli mimi sio mtu
Kila aliyekuchezea apokee mapigo, kila aliyekuonea, aliyekunyanyasa ni zamu yake leo kunyanyaswa. Kila aliyeonea Taifa hili ni zamu yao kuonewa.
Mataifa yaliyopokea siloamu yamepokea chochote walichokuwa wanahitaji.
Muwapelekee salamu hizi;
Rais wa Malawi amelikubali kanisa na cheti tayari. Shida yoyote iliyowapota Malawi leo ni mwisho.
MUNGU amekuja mwenyewe fullfull. Wimbo - amekuja mwenyewe MZEE WA SIKU kuongoza kanisa, kuangamiza vibaya wabaya wote.
Tunayabariki haya mataifa matatu maana yamempokea MUNGU mwenyewe mzima mzima.
Nimeambiwa Kenya, Rwanda watasaini, Botswana wanamsubiri wakamkabidhi cheti.
Uganda wamemwambia amalizie ujenzi wa vyoo wampe cheti.
Mozambique wanamsubiri kuh wakamkabidhi cheti, Zimbabwe kuhani aende akachukue cheti tayari.
Ila hawa niliokamata cheti chao hapa wabarikiwe, na hawa watakapopata shida yoyote  hata wasipige simu wainue hiki hiki cheti na hiyo shida itaishia hapo hapo; nchi ya Malawi, Zambia na South Africa.
Ibada hii imeangusha ukuta wowote uliokuwepo kati yetu na MUNGU,
MARKO 7:20-23    Ili upokee huu moyo uliokuja leo , uliopokea leo lazima ukubali au unatakiwa kusamehe na kusahau.
Uwe na moyo wa rehema na neema ya kusamehe bila kuombwa msamaha.
Ili ujue kuwa umehama ama hujahama  unatakiwa ukiona bado unashitaki wengine, una hasira, unakwazika tu, unazira safu kwa sababu umesemwa, bado unagaragara ukitaka uonewe huruma kwa mahali unapopita , unaona makosa kwa wengine.
Ukiona bado unaona majaribu mpaka leo ujue hujasamehe na hujahama, majira hii hatuna majaribu bali tuna mtihani.
KUMBU 8:2  Test Heart Hutaishi kwa mkate tu bali na kwa NENO linalotoka madhabahuni.
“CHETI cha kusamehe kuachilia na kusahau kanisa tumepewa.
Cheti hicho natakiwa nikiandae vizuri na nikipambe halafu nikining’inize sebuleni pale, chumbani kwako, jikoni hadi bafuni ili kila wakati kikumbushe kwamba umesamehe na kusahau.
Kazi ya kuhukumu ni ya MUNGU”  alisema Wakili wa MUNGU.
Mtihani anatoa MUNGU anafanya yeye anasahihisha yeye na anatoa maksi A+. 
Kila askofu, mchungaji, shehe, padre, watakuwa wanazungumzia SILOAMU.
Najua kuna wengine sasa hivi wameacha kula kwa vijiko huko lutherani na rc.
Kkkt wana morning glory, wana maombi ya kupatana , Je wametoa wapi hiyo ??? SILOAMU!!!!.
Sasa swali langu ni moja je tungekataa kutukanwa kusemwa vibaya? Haya yasingetokea.
Hivi ni kweli unaweza kuanza sekondari bila mtihani, unaweza kuingia  chuo bila mtihani?
Mniambie leo je wasomi unaweza ukawa doctor mwalimu profesa  bila mtihani? Unaweza kupataa phd diploma digrii pasipo mtihani?
Unapokutana na mtihani kwanza kabisa shukuru MUNGU kwa promosheni,utaona jinsi MUNGU atakavyotenda.
Atafanya yeye mwenyewe, atasahihisha yeye mwenyewe, maana mtihani katoa yeye na ni lazima upate A+.
Wale wanaonichukia ni wale watoto wanaopenda kila siku kurudia rudia mtihani na MUNGU anasema utarudia mpaka utakapokuwa mzee.
Maana kama unakimbia mtihani kuzeeka kwaja kwako.
Mtoto yeyote asiyependa mtihani sio mzuri maana anapenda kumaliza hela tu kwa ajili ya ADA maana anarudiarudia darasa.
Unapotoka ibadani kabla ya ibada kwa sababu unawahi appointment ina maana hutaki mtihani unakimbia mtihani.
ISAYA 55:1  UKIONA ISAYA 55:1 haikupi shida ujue umetoka na moyo wa MUNGU leo.
MWANZO 2:5 wakati MUNGU anatamka hayo yote hapakuwa hata na karamu lakini alijua tu kwamba kushiriki karamu damu, kuvaa, kupendeza, nyumba mtaji.
Leo ondoka ukijua wewe ni tajiri kuliko Trump.
YOELI 3:10 aliyedhaifu na aseme kuwa yeye ni hodari. Kama uliambiwa leo unkufa basi ujue na uone kuwa wewe ndiye unaetakiwa kuishi milele hutakufa.
Kama ulikuwa na chumba kimoja leo ona kuwa una gorofa, kama ulikuwa na jembe moja ona leo una trecta,
Kama ulikuwa unashitakiwa kila mahali,unachukiwa, unakataliwa, na mpaka kuna vikao vinavyoendelea kwa ajili yako vya kukufukuza leo nataka uone kuwa unapendwa.
Iko njia mahali pasipokuwa na njia ISAYA 43:16 
Dada mwenye miaka 60 70 80 hata 100 nataka uone kuwa umevaa shera maana ISAYA 34:16 Inayosema hakuna atakayekosa kuwa na  mwenzake.
Hata hivyo pamoja na yote hayo hakuna mwenye miaka 100 wote tuna miaka 6 tu! Wewe uliyeambiwa ugonjwa ulio nao huwei kupona leo uone kwamba umepona MATH 10:1 na LUKA 10:1
JE UMEPOKEA MOYO MPYA LEO? JE UNAJISIKIAJE?
Aidha Kiongozi wa Makuhani Kwenye ibada ya pili alisema tunaona kumbe moyo ulikuwa na vyumba 2 kimoja cha mema na kingine cha mabaya. 
Hivyo hakuna asiyejijua jinsi alivyo kama wewe ni kahaba unajijua, kama wewe ni mwizi unajijua kama wewe hujasamehe hujasahau unajijua vizuri.
Wala usiseme mimi sijijui nilivyo je hujui rangi ulio nayo hujui vazi la kanisa ni nini?
Hivi unapoenda hospitali daktari akasema nimepima nimeona wewe ni kanisa wakati wewe ni kichwa utakubali? Hapana
Atakuambia nimepima mara 3 je utakubali wewe ni kanisa wakati wewe ni kichwa?
Je utakubali wewe ni kichwa na upo madhabahuni ukiwa na shera? Hiyo haiwezekani.
Uwe na hakika ya NENO safari hii hakuna sogea tukae.
Ni magari ya zamani sana yalikuwa yanaitwa chai maharage ndio yalikuwa na hiyo kanuni ya sogea tukae hata hivyo kwa sasa hayapo tena.
Hivyo tengeneza moyo wako leo usiwe na wale wa sogea tukae.
MCHUNGAJI MMOJA AMEKUPA MOYO WAKE ISAYA40:28-31 ISHI HIVYO ILI USIKUTWE NA EZEKIELI 28:18.

Ijumaa, 27 Januari 2017

THAMANI NA FAIDA YA KUWA NA MOYO WENYE AKIBA NJEMA

MITHAL  4:23 linda sana moyo wako. ISAYA 57:15 MUNGU anakaa kwenye moyo uliotubu na kunyenyekea. Yer 29:11 Mawazo ya MUNGU ni mema kwetu siku zote.
Tunatakiwa tuwaze yaliyo mema kama MUNGU KRISTO na WAKILI wa MUNGU WALIVYO. ISAY14:13 Mawazo ya shetani kerubi ni mabaya siku zote.
EZEKIEL 28:17 Ukiwa na mawazo mabaya unakuwa na akiba mbaya ya moyo wako.
Moyo ndio unateketea  na vitu vyako moto unaotoka ndani yako ndio unaua kila unachokifanya.
Mt 7:20-23 Kilichoko ndani ya moyo wako ndicho kinachokupa kuonekana ulivyo, moyo wako ukiwa na akiba mbaya huwezi kuona umuhimu wa mwingine wala huwezi  kusifia au kukubali kazi ya mwingine.
LUKA 6:45 Mtu mwema katika akiba yake hutoa matunda mema na mwenye akiba mbaya hutoa matunda mabaya.
Leo tunamwambia MUNGU kama kuna chochote kibaya kinachotoka ndani  yangu kinachotokana na akiba mbaya ya moyo wangu ukiondoe.
Aidha leo tumetoa Sadaka Maalum ya kufuta akiba mbaya ndani ya Moyo wako, kwa wenye haki, na kwa kanisa.
Sadaka hii inasimamisha akiba njema ndani ya moyo wa kanisa na kwa mwenye haki mmoja mmoja.
Akiba mbaya ni hatari mno katika maisha yangu. Akiba mbaya ndani ya moyo ndio husababisha moto utoke ndani yako na kuangamiza maisha yako au familia yako au kazi zako.
Lakini pia Sadaka hii maalum inafuta kabisa akiba mbaya ndani ya wenye haki kwa kusimamisha nuru zaidi ya Isaya 45:7 ambapo MUNGU kwa uhalisi kabisa anaumba nuru na ana huluku kabisa giza ndani yetu.
*AKIBA MBAYA NI UCHAWI ULIOKO NDANI YAKO MWENYEWE.*

Unatakiwa usimwangalie mwenzio kuwa ni mchawi, mganga,  msengenyaji, ana tabia mbaya.
Yesu alisema usiangalie banzi lililopo ndani ya jicho la mwenzako wakati kwako kuna boriti, toa kwanza boroti ndani ya jicho lako ndipo ukalitoe banzi ndani ya jicho la mwenzako.
Moyo wenye akili mbili, Leo tunaenda kuona akili mbili ndani ya moyo. Akili zinakaa kwenye moyo, akili zipo zinazotokana na moyo wenye akiba njema.
Kuna akili zinazotokana akiba mbaya, na kuna akili zinazotokana na akiba njema ndani ya moyo.
Sasa kumbe akili zinatofautiana, kuna yale uliyosikia na uliyoyaona wewe mwenyewe  hayo hutengeneza store, hifadhi na akiba ndani ya moyo wako.
Unapowaza unawaza kile kilichopo ndani ya moyo wako na kilichoingizwa ndani ya akili yako.
KUMB 8:5 Nawe fikiri moyoni mwako, kufahamu una akiba gani ndani ya moyo wako/wake/wangu.
KUMB 8:2 Nawe utaikumbuka njia yako ambayo BWANA MUNGU wako alikupitisha ili ajue kilichoujaza moyo wako.
MUNGU alikuacha uone njaa, kiu, shida, taabu, aibu ikupate akuone umejaza nini ndani ya moyo wako.
MUNGU anakupima kwa kipimo chake kimoja cha moyo (tester).
Anakuacha ulale na njaa, kuna wakati unawasha mpaka shukrani unaikataa njaa na unasema njaa imefutwa kwa wenye haki kumbe MUNGU ndiye aliyeweka hiyo njaa ndani yako.
Anafanya hayo yote aone kama utaendelea kushika njia zake au utaacha.
MUNGU hawezi kukuacha huru mpaka akupime kwanza aone kama unaendelea kumpenda au umepata wengine wa kuwapenda.
Kumbe kuna majira ambayo MUNGU anakutest moyo wako. Kuna  testa ya akiba njema na akiba mbaya.
Anakutesti kwa njaa au kwa namna yoyote apendavyo MUNGU.
MUNGU anajaribu moyo sababu yeye siku zote huangalia moyo.
MUNGU anakutweza kwa njia yoyote ile ili aone moyo wako.
KUTOKA 14:1- MUNGU aliwajaribu wana wa Israel hata wakae miaka 40.
Hata kipindi cha miezi 6 wapo waliolaumu kwa kuwa MUNGU alikuwa anatupitisha kwa kututweza ili aone, Je unampenda au ndani ya mioyo yetu kuna akiba njema?
Israeli walijaribiwa na MUNGU  kidogo tu pasipo kujua kwa ni MUNGU anawajaribu maneno yaliwatoka, malalamiko, manung’uniko, mpaka wakakumbuka nyama, wali,  pilau na vituguu saumu vya kwa farao.
Kuna saa MUNGU anaruhusu jambo lolote likupate ili aone, Je moyoni mwako kuna nini kimeujaza moyo wako? kwa kuwa kila mmoja huyanena yaujazayo moyo wake.
Walimlaumu Musa mpaka wakasema Yupo nje ya reli  nini mbona tunaona mambo yamezidi, mafunuo yamezidi “as if” utafikiri wao wanaijua hiyo njia.
Maswali ya malaumu kibao wengine wakasema kapotea, mbona tunaomba MUNGU hajibu kumbe wapo kwenye examination na wamekutwa na akiba mbaya ndani ya moyo.
Unamuwazia jambo baya mwingine hata hayupo ila sababu moyo wako umekaa kujihesabia haki tu huoni kama unakosea leo tutubu na tuache.
Leo MUNGU unaona amekuja kuondoa akiba mbaya ujue kwamba  ina maana kwamba kanisa tumeshavuka tayari.
Je unapoona unatoka Madhabahuni au kazini ukakuta vyombo vyote vimetolewa nje na mwenye nyumba kashaweka kufuli lake huku anasema sifungui bila hela yangu  ule wimbo wa naona memaa… unakuja kweli au kitu kipi kinatokea?
Kanisa unakuta kichwa wako yuko na kahaba na hashituki anaendelea tu na mabusu hivi unakuja ule wimbo wa naona memaa….
Leo tujifunze kwa Wakili wa MUNGU;  7abibu 6 alikujaa na gitaa akasema leo ni siku ya kuimba kucheza kuruka maana wengi walisema siku hiyo ni Judgementday wakiimba na kucheza……
Yoh 21:13 Habari za kutwezwa zilimpata Petro akaamua kurudi kuvua samaki. Petro alifanya hivyo kwakuwa alikuwa na akiba ya kuvua samaki.
Ilibidi aondoe akiba yote ndani yake abaki na akiba ya MUNGU tu!!
ISAYA 49:15 MUNGU amesema mwanamke hawezi kumsahau mwanae, Lakini  MUNGU hata akikutweza hawezi kukusahau.
Kwa hiyo ramani ya kanisa MUNGU aliijua tangu zamani kuwa siku ya leo tutafika hapa kwa kuwa  alituchora kwenye vitanga vya mikono yake.
MUNGU alijua leo utavaa vazi ulilovaa leo, utawaza unayoyawaza, utakaa ulipokaa leo na utaelewa somo kwa viwango ulivyoelewa kutokana na akiba ya ndani ya moyo wako ikoje ni ipi.
Unapokanyagwa ni makusudi ili tuone moyo uliokuwa nao yaani MUNGU karuhusu kabisa!!!
Leo ukipata mtihani unatakiwa umshukuru MUNGU.
MUNGU kuna wengine aliwafanya wawe akina farao ili tuwe imara katika imani.
Kwa hiyo  kizazi hiki hatuna majaribu bali tuna mtihani.
[A] Uwe na msamaha kila wakati. Usikumbuke yaliyopita, uwe mwepesi wa kuachilia na kusahau haraka.
Usiamke nalo na ukafika nalo wajibu ukashinda nalo ukarudi nalo huo sio moyo wa MUNGU.
Katika moyo wa MUNGU ni kuwa  na msamaha 1Sam 1:12 Unatakiwa kusamehe kuachilia na kusahau yote.
*UKIWA NA AKIBA MBAYA WATU HAWAKUONI VILE UNAVYOJIONA KWENYE KIOO.*
Hana alikuwa akiomba lakini akiwa hajasamehe wala kuachilia hivyo mbele za MUNGU alionekana ni mlevi wa kutisha.
Ukiwa na akiba mbaya ndani ya moyo wako kila unachokifanya  chochote kinakufa pia unaonekana kitu kisichofaa.
Utakuta mwalimu ametoa swali 1+1 na umeweka jibu 2 lakini akisahihisha akaweka kosa sio kwamba kakosea yeye kaona 4 kutokana na akiba ya moyo wako. Leo tubadilike MUNGU ametuvumilia mno.
Kuna mahali unatembea unajiona binti mrembo mzuri kumbe wote unaokutana nao unaoonana nao wanakuona wewe ni kijana au babu au bibi nk. Sura yako imerejea leo.
Moyo ndio huwa unapika, kichwa wako anaposema chakula ulichopika ni kibaya ni kwa sababu ya moyo wako ulioubeba.
Kila siku anakuambia upike kama Fulani ni moyo wala sio kwamba huyo Fulani ni hawala wake hapana, leo badilika.
Unapika huku unaongea sana karamu huwa mbaya,  pika karamu kwa toba shukrani na imba na kucheza uone kama hajafurahia karamu yako.
Ukimpa shamba mwenye akiba mbaya mazao yote yanaoza, ukiuza dukani duka lote linafilisika na hajaiba na mahesabu yapo vizuri, ukimpa kitu wote wanakufa na wengine anawala yeye mwenyewe kituo hakiongezeki.
Moyo wenye akiba mbaya ni moyo usiozaa, ukiomba nao mito ya shukrani inakufa, ukimpa mwenye haki amlee anamuua, ukifanya nae biashara inakufa, hata ukimpa bilioni tilioni zote zinaisha zote bila kufanya chochote cha maana.
[B] Kibali, kiwango cha kibali unachokuwanacho kinatokana akiba ya moyo wako. Kiwango cha akiba njema ilioko ndani yako Zab 119:1-
[C] Kumcha BWANA  ukiwa na akiba njema moyoni mwako ndipo unaweza kumcha BWANA.
[D] Nguvu ya kutamka jambo likatokea, Kung’oka kwa mlima mbele yako kunatokana na akiba iliyoujaza moyo wako MARKO 11:23
[E]  Hakika ya NENO, War 10:9-10 Kwa kadri ulivyokuwa na hakika iliyojaa ndani ya moyo wako  hukiri na kupokea yale uliyokusudia kupokea. 
Isaya 55:11 MUNGU anasema kuwa kama mvua isivyorudi juu mawinguni ndivyo NENO analolituma kwangu lilivyo kwamba lazima litimizwe sawa na kusudi lake, halirudi bure.
Aidha tumeshiriki Karamu ya Akiba njema ambayo ni Sheria ya Roho wa Uzima.
MWAMBIE MCHUNGAJI MWEMA AKUPE AKILI YAKE ISIYOKUWA NA PANDE MBILI !!!!!

AKIBA NJEMA NI IPI NA AKIBA MBAYA NI IPI?? MITHALI 4:23

Kusimamisha akiba njema ya moyo inayofuta akiba mbaya zote ndani yaa moyo. Moyo una pande mbili.
Kuna chumba kinachohifadhi akiba njema na kingine kinahifadhi akiba mbaya. Tumepewa Moyo halisi ingawa haya yako kwenye Moyo mmoja.
Chemichemi ya uzima inatoka  kwenye moyo wenye akiba njema. Linda sana moyo wako kuliko yote uyalindayo.
Moyo ni store na ni hifadhi ya wanyama wadudu na ndege, majoka pundamilia.
Huu moyo unahifadhi mabaya na mazuri kwa wakati mmoja na ninao moyo mmoja.
LUKA2:18-19  wote waliyasikia maneno hayo lkn mariamu aliyahifadhi moyoni mwake maneno yale.
LUKA 6:45 Mtu mwema katika hazina ya moyo wake hutoa yalio mema ktk moyo wake.
Kadhalika mtu mwenye hazina mbaya katika  moyo wake hutoa mabaya katika moyo wake.
Yote haya yanatokana na kiwango chako cha yale uliyo yasikia na kuyaona.
Maana kila uliyoyasikia yanakaa katika moyo.
Kuna mambo ambayo uliyakokota tangu ukiwa tumboni mwa mama yako tokea siku uliyotungwa mimba kuna uliyoyakuta na yakaendelea kuwepo hapo yakiongezeka kila siku mpaka siku unazaliwa.
Ukiwa tumboni mwa mama yako  kuna ambayo ulikuwa unayasikia yalemama yako anatendewa hata ukayaweka ndani ya moyo wako kwa kuwa moyo ndio hifadhi ya kila ulichosikia na kukiona.
Hii ndio sababu ukizaliwa tu lazima ulie kutokana na yale unayoyajua kuwa yapo ndani ya mji unaouendea.
Kila anachopatwa mama na wewe unapatwa hukohuko tumboni ; mfano, mama akiumwa na wewe unaumwa, akiongea mabaya, akitukana akisengenya, akipigwa, malalamiko, manung’uniko.
Kuna mwingine tokea mimba alichukiwa akakataliwa na baba ukiuliza kwa nini anakuambia ilikuwa si majira niliyokuwa nimepanga kupata mtoto, amenivurugia mipango yangu.
Hivyo mpaka siku akizaliwa mtoto anajua kuwa baba hanipendi  wala hawezi kupatana au mama hanipendi, mama hata kunyonyesha ananyonyesha tu huku akisema sina jinsi ndio hivyo kashazaliwa.
Kuna mjomba, shangazi, babu, bibi walimchukia mama akiwa amebeba mimba au ujawepesi angu hivyo hata nikizaliwa siwezi kupatana nao automatically pasipo hata kuambiwa yaliyowahi tokea nyuma,
Hata wakijifanya kukupenda taa nyekundu inawaka ikisema hawakupendi hawa tokea ukiwa tumboni mwa mama yako.
Pia kuna wanaozaliwa na uchungu na kukataliwa huu ni msingi uliokutana nao ukiwa tumboni uliotangulia.
ZABURI 11:3  Kama msingi ukiharibika mwenye haki atafanya nini? Kwa kuwa tangu zamani ukiwa tumboni mwa mama yako ndiko msingi wako ulianzia halafu ukaharibika, Je ukikua utafanya nini?
Je chumba cha moyo wako kinahifadhi gani? Kuna wenye chumba cha mataarifa ya kusikia, mataarifa ya namfahamu huyu vizuri hadi kwao na tabia zao.
Wengine wengi nafsi zao zimekuwa kama gari la taka, mavi linavuta mitaro.
Kiwango unacholinda moyo wako usiingiwe na mambo mabaya ndicho kiwango cha akiba njema kilichoko ndani yako.
Nafsi ya mtu haili itakula jeuri yake. MITHALI 13:2- Kila mtu atakula matunda ya kinywa chake, kwa kuwa kinywa hunena yaujazayo moyo wake.
MARKO 7:20-23 Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi, maana midomo ya mtu hutoa unajisi matusi ujinga na upumbavu lugha mbaya tu!
EZEKIEL 28:17-18 Nimetokeza moto ndani yako nao umekuteketeza umekuwa majivu najisi kitu kisichofaa.
Moto uliokula biashara yako, kazi, agano lako, nk ni moto ulioko ndani yako wewe wenyewe.
Moto ulioko ndani yako ulioutengeneza kwa chuki  jeuri nk ndio unaosababisha ukwazike, unaovuruga agano lako, unakufarakanisha na kichwa wako, ndio uliokufikisha hapo ulipo wewe katika kila eneo.
Moto uliotokeza ni ile akiba ya ndani ya moyo wako, kile ulichokijaza kwenye moyo  kama kinatokana na maneno au NENO.
Kama una akiba njema  basi utakuwa na mema tu!! Kama ilikuwa akiba mbaya ndani ya moyo basi utakuwa na mabaya tu.
Store ya mambo mabaya akiba mbaya ni moyo wako wewe mwenyewe hiyo ndio imekuteketeza hata huwezi kuwaachilia wengine huwezi kuwatoa ndani ya moyo wako huwezi kuwasamehe na kusahau;
Ndio imekufanya kuwa majivu najisi na kitu kisichofaa, kitu kibaya, ukifanya kazi unajiona house girl, maswali maswali ya kwa nini mimi tu?
Akiba mbaya ndio inakufanya uone unanyanyaswa na kichwa wako, hata kama unaambiwa kweli unaona unadharauliwa, huheshimiwi, kumbe limoyo lako wewe mwenyewe, unasema kila siku unanikwaza kitu kidogo tu hasira umefurai yanakutoka kama umemeza betri leo hama kituo hicho.
Kazi ya akiba mbaya ni kutoboa madirisha kwenye moyo wako ili aje akuibie:-  
+nguvu,
+Uweza,
+Baraka,
+hekima,
+heshima,
+utukufu na                                                               +utajiri.
Akiba mbaya analeta ukimwi kisukari ili ujue kama ni akiba mbaya utasikia doctor anasema usiwaze sana, usipaniki, usikasirike kasirike, usikwazike, manung’iniko yote haya husababishwa na akiba myaya ndani ya moyo.
Kwa hiyo ujue akiba ya MOYO wako ndio inayokupa maisha ya kuishi. Akiba mbaya hufungua milango ya mabaya na kukuletea mauti.
Huleta magonjwa, ukiwa na vidonda vya tumbo ujue una akiba mbaya ya moyo wako. *DALILI ZA AKIBA MBAYA;*
#Magoti kulegea,
#mabega kuchoka,
#mgongo kuuma, 
#kiuno kuuma,
#miguu kuwaka,
#kujisikia kununa saa zote,
#vidonda vya tumbo,
#kukosa hamu ya kula kitu chochote,
#kutokuwa na amani wakati wote,
#macho kupungua nguvu ya kuona,
#kukosa usingizi au kusinzia sana,
#kutembea huku unaongea peke yako mwenyewe mpaka unaamua mwenyewe,
#kupenda kujieleza sana .
#Kutojiamini ,
#hisia mbaya kila anayeongea anakusema wewe,
#kukosa furaha saa zote,
#hata ukivaa hupendezi, #hakuna hata siku moja ambayo unambiwa umependeza, #unafilisika tu huongezeki, #unaharibu mahusiano yako na MUNGU na unakufarakanisha na kuoa kuolewa fedha, kazi,
Inakula mifupa ,
#ndio unaokuchafua, unaokutaabisha, unamuangamiza, unakushusha chini, unakufedhehesha, unakukosesha na kazi nzuri,
#kila unachoongea ni kibaya.
Je hujawahi kuona mwenye diploma anapata kazi nzuri lakini mwenye digrii mfagiaji tena anapewa kufagia nje? Sababu ni moyo.
Badala yakuwa na moyo wenye kutoa chemichemi ya mambo mazuri unakuwa ya kutoa mabaya.
Dalili hizo ni pamoja na; uso wake hukunjamana ,kuwa na hasira saa zote, ana maswali yasiyo na majibu, kuwa na hofo, woga hata kupanda pikipiki tu utakikia anaogopa kufa, kuota ndoto za kufukuzwa na wanyama, kutomwamini mwingine.
Kutokuwa na moyo wa shukrani, kutokuwa na furaha hata ufanyiwe nini,huoni mema kwa wenzako yote ni mabaya tu, hata uimbe vipi naona mema aa naona mazuri tu ….. akiba mbaya anakuzomea maana anajua unadanganya kupritent!
Hupati tenda kwa sababu ya moyo wako… unapoandika application sio yale maandishi yanayokua kazi tenda tena bosi anaposoma hasomi lile karatasi bali anasoma moyo wako ndio sababu hupati unachotaka.
Unapaka cream ili uonekane mzuri, kuwa na machunusi usoni, ngozi inakubabuka, umeoauka  midomo inakauka na kupasuka.
Ni mkali cku zote kitu kidogo tu anashikilia bango, akitembea utasema ni mnyenyekevu kumbe amejaa akiba mbaya tu!
Kila unachofanya ili kipate kibali au kikose kibali ni kutokana na akiba uliyonayo.
Kuna moto unaotoka ndani  ya kila mmoja unasababisha uwe kitu kisichofaa mbele za MUNGU na mbele za wengine.
Leo kila tabia uliokuwa nayo au moyo uliokuwa nao wenye akiba mbaya unatolewa.
MAMBO YANAYOSABABISHA AKIBA MBAYA;
*Kufukuzwa kazi kwa kuonewa kwa ghafla,
*kuna jambo ulilolitarajia likachelewa kutokea,
*kuna majibu mazuri uliyoyategemea yakajibiwa vibaya,
*kuna matokeo mazuri uliyategemea yakaja kinyume visivyo,
*kuna uliyemtegemea akakuacha kwa ghafla,
*uliyemuamini sana akakuasi,
*akakugeuka, akakusaliti,
*akakutenda ubaya,
*ulitenda mema ukalipwa mabaya,
*kufiwa ghafla na uliyempenda,
*aliyekupenda,
*uliyemwamini,
*ukamwamini,
*Tendo au matendo uliyowahi kufanyiwa ukatili,
*kubakwa kulazimishwa kufanya mabaya,
*kuugua kwa muda mrefu,
*kuuguza kwa muda mrefu na kwa gharama kubwa halafu asipone akafa,
*kupita mahali pagumu kukosa fedha,
*kusalitiwa na uliowaamini,
*waliokuwa karibu na wewe.
*na mambo mengine hayo yote yanayoleta kuwa na akiba mbaya ndani ya moyo  wako.
*Aidha kuna madeni yasiyolipika ,
*kudaiwa kwa vurugu mfululizo.
*Kesi za kusingiziwa,
*kusingiziwa umezini,
*unaiba na uchawi hizi ndizo kesi ambazo huleta shida mara nyingi pia huleta akiba mbaya.
*Na wengine huchukua uamuzi mbaya mno, hatua mbaya.
Tunatakiwa tuwe na moyo wenye akiba njema pekee.
Homework ; kila mmoja kuanzia leo akutane na mwenzake au kuhani ili ufunguliwe ili kuondoa akiba mbaya zote ndani ya moyo kwa siku saba. Pia katika wiki hii hutakiwi kukosa ibada za majibu.
CHUNGAJI MMOJA LEO AMETUKUTA NA AKIBA MBAYA KILA MMOJA AONDOE ILI APATE  PA KUKAA.
POINT: EZEKIEL 28:18{b}

Jumatano, 25 Januari 2017


SIKU 7 ZA KUKABIDHI MOYO MMOJA HALISI KWA MUNGU ALIYETUMA WOTE VIZAZI VYOTE

Kushukuru MUNGU kwa ajili ya mwezi tammuzi uliotupa moyo mmoja halisi. 
Moyo  ambao umetupa Kweli Halisi inayotupa kuishi na MUNGU na inatupa kuchungwa na Mchungaji mmoja Halisi.
SADAKA; Kufuta chochote chochote kilichokuwa kimekaa  kwenye moyo wangu na kuondolewa ngani yangu, Kanisa kwa wenye haki na kila kinachoitwa kwa jina langu.
ZABURI27:4 Sadaka hii inanipa mimi kukaa kwenye Neno sawa na ninavyofundishwa kwa uzuri wa MUNGU, Nifurahie na kutafakari  ambayo MUNGU ametenda kwetu Kanisa.
Mwezi wa tammuzi tumepewa Moyo mmoja Halisi, MUNGU anachoangalia ni Moyo wake ndani yangu, Moyo ambao ndani yake hakikai wala hakai yeyote zaidi ya MUNGU peke yake.
Ukiweka kilimo ndani ya Moyo, siku ya kupanda  unasema napanda kwangu kwanza kwa MUNGU baadae.
Huu sio moyo mmoja unatakiwa kumuweka MUNGU kuwa namba moja   kwako.
Hakikisha hufanyi chochote kilicho chako kabla kufanya kwa MUNGU.
Na sasa unatakiwa ujenge tabia ya kujenga au kupanda kwanza kwa MUNGU kabla yako.
Ifike mahali  pa kusema MUNGU kwanza vitu vingine baadae.
Unatakiwa uwe na Moyo mmoja Halisi sio mioyo mingi, mioyo ya vitu vingine ndani yako.
Matendo13:22 WAKILI WA MUNGU siku zote anatenda anafanya yaliyo mapenzi ya MUNGU peke yake.
Tunaona hata kizazi cha pili Daudi aliyatenda mapenzi ya MUNGU.
Leo mimi mwenye haki ndiye ninayetakiwa kuyatenda mapenzi ya MUNGU ndani ya kizazi chake.
ZABURI 89:1- Ni Daudi peke yake ambaye MUNGU amesema kuwa kiti chake kitakuwa cha MUNGU kwa kuwa aliyatenda mapenzi ya MUNGU kwa sababu ya Moyo mmoja ndani yake.
Kiti kuthibitika, Moyo wa MUNGU unakupa kushinda  kama WAKILI wa MUNGU alivyoshinda na zaidi ya kushinda.
KUMB5:29 Laiti wangekuwa na Moyo kama huu siku zote wa kunicha wangefanikiwa wao na watoto wao yaani [uzao] MUNGU anasema ukiwa na Moyo wake ndani yako utafanikiwa.
Kinachozaa ni Moyo kwa hiyo usipokuwa na Moyo wa MUNGU unazaa mambo ya Moyo ulionao sawa na ulivyopanda  utavuna hivyo hivyo.
Math12:33-35 ili uzae lazima uwe na Moyo wa MUNGU unaozaa vitu vizuri.
Hata ukisema tasa ni Moyo wako ndio tasa lakini kizazi chako ni kizuri ila kwa sababu Moyo ni chanzo cha vitu vizuri kama haupo vizuri huwezi kupata mtoto.
Madoctor utakuta wanahangaika na pracenter akijua ndio tatizo lilipo kumbe tatizo lipo kwenye moyo wake mwenyewe maana kinachozaa ni moyo sio pracenter.
VITU VINAVYOKAA KWENYE MOYO:- Moyo umebeba yafuatayo;-
#Nguvu ya udhihirisho,
#Nyota ya mambo mazuri [MAFANIKIO].
#Moyo ni mtawala wa vitu vyote.
#Ndani ya huu moyo wenye vitu vizuri anahitajika akae  MUNGU peke  yake.
Katika NYOTA KUNA;-
*nguvu,
*hekima,
*Baraka,
*utukufu,
*heshima,
*uweza,
*utajiri.
Moyo ukiibiwa ujue vitu vyote hivyo utavipoteza.
Pia jua kwamba akija mwingine kukaa ndani ya moyo vitu vyote vinakimbia hata ulivyokuwa umeahidiwa hupewi tena.
Ndio sababu MUNGU anasema linda sana moyo wako kuliko vitu vyote uvilindavyo Mith 4:23.
ZABURI32:1- Neno linasema heri aliyesitiriwa dhambi zake yaani heri anayesamehewa dhambi, Daudi alieleza moyo wake jinsi usivyomficha MUNGU. 
Wenye haki hatutakiwi kuruhusu moyo kubeba uchafu ndani yetu, siku zote tutafakari ukuu wa MUNGU.
1nyakat29: Daudi alikuwa ni mtoaji kwa viwango visivyo vya kawaida, sadaka alizokuwa anatoa zilikuwa zinaonyesha moyo wa MUNGU ndani  yake.

MUNGU anataka kila mmoja awe na huo moyo wa MUNGU ndani yake.
Kila kitu unachofanya ufanye kwa ajili ya MUNGU kama WAKILI WA MUNGU anavyofanya. Tujifunze kwa mtini .
WAKILI wa MUNGU hakuwahi kumtolea MUNGU kitu kinyonge, je sisi tunatoa wapi?
Tunatoa vitu vingine hata sisi wenyewe tukipewa haturidhiki na hata tukipata wengine tunavitupa au kugawa kwa wengine, leo tubadilike.
Leo unatakiwa uondoe chochote kinachosababisha usimuabudu MUNGU kwa Roho na Kweli.
Unapoona Kichwa,  Kanisa, watoto, biashara, shamba, nyumba  anasababisha usije hata ibada za majibu usimtolee  MUNGU ujue vipo ndani ya moyo wako leo uwaondoe na uviondoe ukatae kabisa.
Jikague kuna mahali unajikuta unaongea maneno mengi badala ya NENO ujue kuwa ni kwa sababu ya walioko ndani ya moyo wako .
Kuna ambao mko hapa lakini kuna jambo ndani ya mioyo ambalo halitoki ili MUNGU akae leo kubali wewe mwenyewe likatae na uyakatae yote uliyowahi kufanyiwa  ambayo mpaka leo ukilikumbuka hata MUNGU Kristo Wakili wa MUNGU unawaambia wakae pembeni kwanza leo kubali kulitoa ili MUNGU akae ndani yako.
MUNGU anaangalia moyo kitu gani ukiguswa unalalamika unanung’unika unakwazika unanuna unakasirika unafura?
je ni fedha, mahali pa juu pa cheo kazi umri fedha kichwa kanisa watoto.
Hivyo kwa sababu wote tumekubali tumekiri kuwa kuna kitu tukiguswa ndani yetu tunashindwa kuvumilia basi yatupasa kutubu.
Leo tunatakiwa tutoe kila kitu kilichokuwa kimebaki ndani yangu/ yako / yetu badala ya Moyo mmoja wa MUNGU.
*MCHUNGAJI MMOJA ANAKAA KWENYE MOYO WENYE AKIBA NJEMA.*

Jumanne, 24 Januari 2017


KWELI IMESIMAMA    KWA UHALISI

Tunashukuru MUNGU kwa sababu sasa Kweli imesimama kwa uhalisi. Kweli ilipotoshwa tangu UF12:1 alipo wa na Kanisa akatokea mwanamke [photocopy].
Tangu mlimani na vizazi vyote vinne kweli ilikataliwa kulikuwa na uongo na alifutwa jana. Mbinu za uovu zilizokuwa zinasumbua wenye haki  zimefutwa.
Tangu siku ya kwanza MUNGU alipoumba mbingu na nchi na kisha kuwakabidhi shamba wakulima kweli haikukubaliwa ilikataliwa.
YOHANA 19:1-20 PILATO alikubali kwa sababu kweli haikuwepo. Damu ya kweli kufuta uongo na ukweli.
Shinikizo limesababisha wengine watoke mahali pao.
Kuna waliofukuzwa kwenye agano lao, leo kiapo kimesimama; kuvunjwa kwa agano la kwa uongo.
Yeyote aliyekuwa anachukua nafsi za wenye haki na kuzitumia kinyume leo ndio mwisho wake.
*MBINU 3 WANAZOTUMIA MASHETANI*
Kwa nini mwenye haki anaadhibiwa?
1.)Muovu kuingia ndani ya nafsi ya mwenye haki na kutenda dhambi.
V Unajikuta unafanya kitu cha ajabu mpaka wewe mwenyewe unajishitukia unajishangaa kwa yale unayoyafanya.
Kuna wakati unajikuta unajiuliza maswali kwamba hivi ni mimi ninayefanya haya yote kumbe ni kutokana na Yule muovu aliyeingia kwenye nafsi yako.
Hali hii ya muovu kuingia ndani ya mwenye haki na kutenda mabaya kinyume na MUNGU kinyume  na Neno ni mwisho.
2.)Muovu kuingia ndani ya bosi wako , mzazi, mlezi, mwanao nk ili kuharibu uhusiano mzuri uliokuwepo kati yenu leo ni mwisho.
Unakuta bosi wako kwa ghafla kabadilika mpaka anatamani akufukuze kazi na wakati mwingine unajikuta unatamani usaini kuacha kazi kumbe ni adui leo ni mwisho.
Mlima wa moto unakutana na watoto ukiwaambia msifanye msiangalie tivi kabla ya kupika unakuta wameangalia mpaka wameunguza karamu.
Kijana, binti unajikuta mzazi wako kila ukipika anakuambia karamu gani hii umepika mbaya namna hii na amekula amemaliza kushiriki leo njia zote za adui kuharibu uhusiano mzuri na madhabahu yake imefutwa milele.
3.)Kuvalishwa mavazi mabaya ya waliokufa, uchawi, uganga, uloz, unajimu, hasara, kudharauliwa, leo yamefutwa.
Haya mavazi yalisababisha hata ukisema kweli ikataliwe leo ni mwisho.
Leo ukisema  kweli na kuonekana kuwa ni mchawi ni mwisho.
Wakili wa MUNGU anapokupa vazi lake ujue kwanza umepokea mafuta yake.
Hii nguvu wachawi walichukua na kuligeuza wenye haki kuonekana wachawi waovu leo mwisho. YOHANA 8:1-
Tabia ya kutafuta kumuua WAKILI WA MUNGU kila siku ni kwa sababu  NENO LA MUNGU halikuwepo halipo ndani yao.
Utasikia sisi ni wa Ibrahimu, Eliya mtishibi, Yesu, Eiya Ad2 lakini wanayofanya hayafanani nao ambao wanawasema ndio sababu Yesu mwasema ninyi ni wa baba yenu Ibrahimu;
Mbona mnayotenda hayafanani na huyo Ibrahimu, Eliya Ad2 maana hata wao wangekuwepo wasingefanya hayo mnayoyafanya leo kwa Wakili wa MUNGU.
Hata wakati wanaongoza vizazi hawakuwahi kumshitaki yeyote, hawakumtukana yeyote, hawakumkosoa MUNGU milele. Nyie mmetoa wapi?
Aliye wa MUNGU husikia na kuyajua yaliyo ya MUNGU na kuyelewa sasa mbona WAKILI WA MUNGU anasema yaliyo ya MUNGU lakini hamuelewi, mnamshitaki  MUNGU.
Ukisoma haya mazungumzo yaliyopo yohana 8 utajua kuwa kweli ilikataliwa siku zote hizo.
Hawataki kweli utasikia wanasema WAKILI tunampenda lakini mafundisho yake hatuyataki tunayataka yale ya baba yetu Ibrahimu,
Eliya Ad2, kizazi cha tatu walikataa mafundisho ya Yesu wakataka ya Ibrahimu yaani mafundisho ya kabla hata ya majira ya 3 ya kizazi cha 1.
YOHANA 19:1-20 Pilato naye hakuijua kweli japo alitamani alipenda kumtetea YESU ktk majira ile lakini haikuwezekana kutokana na kutoikubali kweli.
Kanisa tuna haja ya kumuomba MUNGU kweli kweli ili Pilato ajue kweli na aikubali. Leo tunaipeleka kweli kwa pilato.
Mpaka sasa serikali haina shida na kanisa na WAKILI WA MUNGU shida ipo kwa wale wanaopeleka taarifa za uongo, barua za masingizio, mashitaka ya uongo, michoro ya mabaya, ramani mbaya  leo tutubu.
Leo kwa sababu kweli imesimama mashitaka yote yamefutwa kwetu milele.
Mashitaka ambayo MUNGU, Kristo Wakili wa MUNGU Kanisa na Taifa wameshitakiwa leo yamefutwa milele.
Nira zote kamba zote zilizokuwa zimetufunga leo zimefutwa milele. Kizazi hiki pilato lazima aijue kweli ili mashitaka yote yaondolewe kwa YESU.
Maagano ya kichwa kanisa yaliyo haribiwa na kahaba leo yamerejea kwenye kusudi kwa sababu kweli imesimama leo.
Kesi za masingizio zimefutwa ila kama ulikuwa na machungwa ya watu kweli nenda ukaseme kweli kwa kuwa kweli imesimama yenye kukuweka huru. Vifungo vyote vimeng’olewa milele.
Roho za masingizio zimefutwa, kuanzia leo utaaminiwa kila akuonae ataona wema wako ulioutenda, uadilifu wako utaonekana, ukifanya kazi utalipwa kwa haki maana kwa kuwa sasa kila utakapofanya kazi utakapoonekana utakuwa KEKI kwenye wajibu wako mlima wa moto, biashara zako.
Kila kazi unayofanya ulikuwa unadharauliwa kuanzia leo utathaminiwa.
Sasa kama ulifanya biashara lakini ikakataliwa leo kaianzishe tena utafanikiwa itakubalika itapendwa itakimbiliwa utaitwa kwenye tenda mbalimbali.
SADAKA maalumu ya leo ni kufutwa kwa mavazi ya mambo mabaya yote, kutokuwa na thamani katika kila kitu unachofanya.
Kusimamisha Kweli ili kuunguza mavazi ya maneno mabaya yote kwa sadaka hiyo.
Pia Sadaka hiyo maalumu inafuta usingiziaji kwa maneno yote ya uongo na mavazi ya usingiziaji kwa wenye haki. 
Kufuta laana zisizo na sababu, kituo cha kufanya kazi kubwa bila malipo.
Mashitaka yaliyokuwa yamepelekwa kwa pilato yamefutwa.
Uongo uliokuwa umeenezwa kwa ajili ya Kanisa umefutwa kwa sadaka. Pilato + kaisari wataijua kweli kwa sadaka hii.
Mavazi aliyokuwa amevalishwa pilato asiijue kweli leo yameuungua yamefutwa kwa sadaka sasa ataijua kweli moja halisi.
*MCHUNGAJI MMOJA MWEMA NA AKUKUTE KWENYE KWELI SASA ILI APATE KUKUCHUNGA.*

Jumatatu, 23 Januari 2017


KWELI MOJA TU IMESIMAMA NDANI YA KANISA NA UUMBAJI WOTE.


Wakili wa MUNGU leo amesimaisha Kweli moja tu ndani ya kanisa na uumbaji wote na kusema “Maisha yangu yote kuanzia sasa hivi yatakuwa na Moyo mmoja, hivyo Moyo mmoja umekuwa ni sehemu ya maisha yangu yote milele.”
Sasa baada ya Moyo mmoja tunasimamisha kweli moja halisi. LEO KWELI INASIMAMA NA UKWELI NA UONGO UNAFUTWA.
Kulikuwa hakuna namna ya kuwa na kweli kutokana na mioyo mingi iliyokuwepo tukajikuta hata ukiambiwa uongo unaona ni kweli lakini leo ndio mwisho kweli itajulikana kuwa kweli na uongo utajulikana kuwa ni uongo.
Kwa sababu kweli imesimama sasa hatutasingiziwa tena, hatutazushiwa tena. Mashitaka ya uongo kwa wenye haki leo yameungua.
Maisha ya mateso kwa wenye haki, masingizio kwenye familia, kuchukiwa kwenye familia yako kutengwa kwenye familia yako, kuonekana hufai kumefutwa hutaona tena maana kweli imesimama.
Sasa utaonekana ni mwenye haki kwenye familia nk.
ZEKARIA8:1 na YOHANA8:31-. Kweli pekee ndio inayokuweka huru kila mahali. Tangu zamani kweli haikuwahi kusimama.
Hata wakati wa YESU kila aliposema kweli waliokota mawe wakitaka kumpiga nayo na wakati huo hata wao wanajiita ni wa MUNGU.
Leo tambua hata wale wote WANAOMKATAA wanaomtukana WAKILI WA MUNGU hao sio wa MUNGU japo wanajiita ni wa MUNGU.
*Kweli ilikuwa haikuwahi kukubaliwa popote.*
Kuanzia leo TUMEAGIZWA kusema kweli tu! Kwa kuwa hakuna wa kuokota mawe hakuna wa kukupiga jiwe milele.
KUANZIA LEO TAMBUA KWAMBA MUNGU AMEKUBALIWA NDANI YA UUMBAJI WOTE KWA SABABU KWELI IMESIMAMA.

ZEKARIA8:1- Sasa kanisa ni mji wa kweli ya MUNGU  na MLIMA MTAKATIFU .
Sasa MUNGU atakuwa ni MUNGU wetu katika Kweli na katika Haki.
Adui alikuwa ni moyo wa pili kwa sababu hiyo  MUNGU aliacha tupigane power chafu lakini leo MUNGU hataacha wakusumbue wakupige power chafu kwa sababu tayari Kweli imesimama.
Mwanzoni tulionekana ni laana lakini sasa hatutaonekana laana tena. Wakati wa natuwasha tulionekana kama vile hatuna MUNGU lakini  sasa MUNGU amesimsmisha kweli yake hakuna wa KUNIGUSA.
Kila mmoja na aseme kweli  na jirani yake. Kila mmoja asimame kwa haki asiape kwa uongo.
Huu ndio mwisho wa kerubi , ibilisi, shetani, nyoka mwamamke, mwanaume, kahaba mkuu, mnyama asiyejulikana sasa KANISA LA MUNGU litajulikana.
Kila mmoja na aseme kweli na ndugu yake . mashtaka yaliyokuwa yamepelekwa popote ya uongo yamefutwa.
Aidha wakili ameongoza wenye haki kutoa Sadaka Maalumu ya Kusimamisha kweli. Kufuta  uongo ukweli. Kufuta mashitaka ya uongo juu ya wenye haki.
Sasa kweli imesimama wengi waliofungwa gerezani wataachiliwa huru kwa sababu wengi walihukumiwa mpaka kufungwa kwa sababu ya mashitaka ya uongo leo mwisho. Mataifa yaliyokuwa yanatumia nguvu ya taifa hili sasa utaona wengi wakiishiwa  wataanguka kwa kuwa kila kitu kinarejea mahali pake.
Sasa hivi ni majira halisi ya KUJULIKANA NA KUTAMBUA kwamba nani alikuwa anamsaidia mwingine /mwenzake. Hii majira ilikuwa inasubiri leo.
Ibada ya jana ilikuwa si ya kawaida ndio iliyotuletea ibada ya leo.  Sasa wewe ambae umeoa  umeolewa badala ya mwingine hapo ndio sijui tumuachie MUNGU mwenyewe.
Wengine tunawaona wamepararaizi lakini kumbe ni mzima ila kuna mmoja anayetumia  upande huo mmoja leo mwisho.
Kuna tuliowaona ni zezeta kumbe ndio wana akili nzuri. Kila aliyekuwa anasoma kwa ajili ya wengine wakaenda juu leo wanafukuzwa vyuoni.
Kila aliyeshitakiwa kwa uongo leo anaachiwa huru. Kweli imesimama kila mmoja atasimama kwa NAFSI yake.

Wengine hapa hawana afya zao sura zao leo zinarejea. 
Haya yote yanatokea kwa kuwa kweli imesimama.
Na ijulikane wale akina mama wenye macho mekundu kule SHINYANGA  kama ni wachawi au laa.
Dini na dhehebu wanasema kuwa SILOAMU ni freemason leo kweli imesimama na ijulikane kama SILOAMU au ni wao dini na dhehebu ndio freemason.
Baada ya kweli kusimama sasa mchawi na asimchawi atajulikana.
Kila mmoja anapokea shea yake kwa MUNGU iliyokusudiwa tangu mwanzo.
Sasa anayesema kweli atajulikana na anayesema uongo atajulikana. Ambae ni mwizi atajulikana na asiye mwizi atajulikana.
SHUKRANI: Kuna kiapo kimesimama *NI MWISHO WA MUNGU, KRISTO WAKO, WAKILI WAKO, KANISA LAKO, TAIFA LAKO NA KIZAZI CHAKO KUSHITAKIWA.*
Tumeinua mnara wa kweli  ambao unasababisha kila mmoja  kuona kuwa SILOAMU ndio wanaosema kweli pekee. Mnara wa uongo uzushi  adui umefutwa.
Hakuna atakae gombana na jirani ndugu yake milele. Mafaili ya kila aina ya uongo yamefutwa.
Leo ni cku ya kukumbukwa mno kwetu. Maana kila nafsi inarudi mahali pake. Kila shilingi dola rasilimali heshima vyote vilivyokuwa vimeibiwa vimerejea mahali pake.
Kila ulichowahi kuibiwa jua leo kimerejea. Mambo ni matamu. MUNGU awabariki awape kila mnachohitaji. 
KWELI NDIO INAYOKUPA KUCHUNGWA NA MUNGU AMBAYE  NDIYE  MCHUNGAJI MMOJA HALISI.

Jumapili, 22 Januari 2017


MOYO MALIDADI KWA UHALISIA NDANI YA KILA MWENYE HAKI.

MUNGU leo ametupa Moyo Toba na unyenyekevu ambao ndio unaotupa kuwa na Moyo Malidadi.
Wakili wa MUNGU akasema pasipo huo unyenyekevu huwezi kupokea huo Moyo Malidadi.
Aidha kabla ya fundisho la leo MUNGU alikuja na ushuhuda wa ushindi wa MUNGU, KRISTO NA KANISA , ushuhuda wa kutisha wa Farasi wa Moto unaoitwa THE POOL OF SILOAM CHURCH.
MUNGU amesema sasa kanisa halipo kwenye yai tena bali hadharani. Akasema mambo haya yanatambulikana kwa jinsi ya Rohoni zaidi.
Kushukuru MUNGU kwa ushuhuda huu ina maana kila mmoja leo alichokuwa anataka amepokea.
Aliyekuwa anataka gorofa, kiwanja, nyumba, gari, kampuni, afya , ufahamu hekima maarifa nk leo umepokea.
Akasema siku ya leo kwa ushuhuda huu chochote ulichowahi kukihitaji leo UMESHAPATA.
Aidha akaonesha kitabu kipya ambacho kina majibu tu ya maswali mbalimbali anayoulizwa MUNGU Aliyetuma wote akasema “KUMBUKA kitabu hiki hakina maswali bali kina majibu tu!
Hivyo hata wewe mwenye haki huna maswali una majibu tu!
Leo hama kituo cha itakuwaje kwa habari ya ada za watoto, kwa habari ya kichwa wangu, kanisa wangu biashara yangu, wajibu wa moto. leo ondoka ukijua una majibu peke yake”.
“Anayetembelea Reli ya rohoni leo anaondoka na majibu peke yake anaondoka na vitu vizuri peke yake” aliongeza Wakili wa MUNGU.
Aidha MUNGU alifurahia uimbaji wa leo akasema HAKUMBUKI SIKU TULIOWAHI KUIMBA VIZURI KAMA LEO!
YOELI 3:16-19; Sasa magonjwa utasa kuzomewa mateso hayataonekana kwa wenye haki tena kwangu kwako milele.
Bonde la shitimu yaani jangwa ukame kukaukiwa kuishiwa kumefutwa kwa wenye haki wala hutaona tena.
Kwa ibada ya leo utakuta account yako imejaa, mlima wa moto utakuta friji limejaa karamu.
leo kila mmoja atapokea zawadi, kila mmoja ataondoka na zawadi yake.
Misri itakuwa ukiwa giza utupu upofu hasara wenye kupatwa na mabaya unyonge utumwa mgumu mahangaiko nk Aliyetamba kwa dhuluma atakuwa ukiwa. Mfuko uliokuwa hauna kitu leo unaondoka umejaa.
Tumefika ile majira ya ukifikiri tu umepokea, kutozaa kwa tabu, huzuni na kuugu vimekimbia kwangu  kwa uhalisi.
MUNGU akasema tuache mshangao muda wa ibada, TAMBUA walishaapa kuwa mwenye haki hatavuka.
*“LEO NAAPA KWAMBA MWENYE HAKI AMEVUKA!!!!”* aliapa Wakili wa MUNGU.
Kulikuwa na madhabahu ya siri iliyokuwa inasababisha kila kitu unachotamkiwa wewe mwenye haki  kizuri kugeuzwa kuwa kibaya , yaani hata utamkiwe NENO tamu vipi unaona kuwa haiwezekani , unaangalia mazingira ulivyolala na njaa jana ulivyopigwa na kutaabishwa na kichwa wako kila siku LEO MUNGU AMEIFUTA HIYO MADHABAHU KWA UHALISI.
Sasa hata hii Madhabahu mahali nilipo ni round sio pembe nne tena , maana huu ni MLIMA WA BWANA hakuna pembe 4. Ni majira ya ISAYA2;2 MATAIFA WANAKUJA hawawezi kufikia kwenye madhabahu ya pembe nne.
LEO, mwambie MUNGU akupe kituo cha kushinda maswali maswali. Unayotamkiwa unaona hayawezekani je hata MUNGU  huna? Je kwa nini sasa usione kwamba umepokea?
Changamka maana kila ulichokuwa unahitaji umepata mtaji umepata. Sema hapa nilipo sina jangwa, sipungukiwi, sifilisiki, sioni majitu, sikati tamaa…. hakuna maskini wote tupo kwenye bustani ya Edeni mpya kabisa.
Aidha Wakili wa MUNGU aliagiza wenye haki kutoa Sadaka maalumu ya kuhukumu mtaabishaji wa Kizazi cha MUNGU.
Yeyote aliyekuwa anavaa vazi la kumtaabisha MUNGU Kristo Wakili wa MUNGU Kanisa taifa kizazi cha MUNGU amehukumiwa kwa sadaka hii.
Nataka ufurahie Vazi Jeupe ambalo maana yake ni kutoka kwenye dhiki kuu.
Leo kila mmoja anashuhuda aliyekuwa anazuia amehukumiwa na MUNGU. Kushukuru MUNGU kwa kuwa mtaabishaji wa kizazi cha  MUNGU amehukumiwa tayari.
Maana ilikuwa ukitamkiwa Baraka anasema laana , ukitamkiwa uponyaji anasema magonjwa, fedha-makaratasi, utajiri-umaskini, uzima-mauti leo amehukumiwa.
Sasa umefika wakati wa kwenda mikumi unakutana na simba wala hana haja na wewe, hii itatokea mtaanza kusikia kwenye vyombo vya habari.
Akizungumzia Moyo Malidadi Wakili wa MUNGU alisema Malidadi ni mpya haujawahi kuwepo ,
leo kanisa tunaondoka na Moyo Malidadi mpya. Malidadi ni zaidi ya malidhawa.
Leo MUNGU amefuta mioyo mingi ndani yetu ili tuweze kupata huo moyo Malidadi lazima tuwe na moyo wa toba na unyenyekevu.
TUNAPATA FAIDA GANI; 1SAMWELI 15:10- Unyenyekevu ni nini na faida yake ni nini? Leo tuondoe moyo wa kujihesabia haki kujitetea. Tunaona bado tuna tabia ya kumdanganya MUNGU.
SAULI alikuwa akiambiwa jambo na MUNGU anakubali vizuri anaitikia vyema kabisa lakini akimpa kisogo tu anaenda kufanya kinyume huu ni ukaidi . 
Bado akikutana na nabii wa BWANA akiulizwa na ametoka kufanya kinyume tunaona sauli alisema kuwa amefanya kama MUNGU alivyomuagiza wakati hajawaangamiza waamaleki wala mfalme wao huu ni ukaidi leo tuhame vituo makuhani wa MUNGU NA KRISTO WAKE.
Tunatobolewa macho kwa kukosa kutenda sawa na tunayoagizwa tunatoka ibadani kwa MUNGU WA KWELI tunarudi kwenye dini na dhehebu, mila na desturi, dhambi uovu uasi na yale tuliokuwa tumeyaacha kwenye mataputapu nk leo tambua GARI LA MUNGU HALINA LIVASI.
Unakosoa mafundisho,husikilizi ibada wewe ni wa siku ya tano hadi ya tano, huji ibada ya majibu huu ni UKAIDI na ujue unaibiwa vitu vyako vizuri.
Kilichosababisha sauli kuwa hivyo ni 1SAMWEL 10:17 MOYO ulikuwa na takataka. 
Hamsikilizi masomo nyie mnataka kuniambia hamna laki 1 ,2 za kununua simu nzuri za kusikiliza masomo?  Je, mnashindwa kumwomba SHOHAMU akuunganishe na GROUP uwe unapata masomo ?
MWANZO 3:1- Adamu alikosa moyo wa toba na unyenyekevu. Kutokukubali kosa .
kujihesabia haki . kujitetea hivyo hata ambavyo MUNGU alimuahidi  alivyokuwa amekuahidia HUPATI MILELE kwa kukosa unyenyekevu na toba.
Vilevile MUNGU anakutupa kwa kukosa unyenyekevu na toba na akikutupa amekutupa. 
Acheni uongo, usiseme ni Fulani kanifanyia hivi hivi kanikosesha … kaa kwenye toba tubu kwa yote.
ISAYA 61:1, Mwenye moyo wa unyenyekevu ndie anayepewa habari njema.
WAKILI WA MUNGU; moyo wa toba na unyenyekevu ndio uliosababisha kila siku kupewa ufunuo mpya , miezi 6 hiyo ilikuwa  sio mchezo. 
YOHANA 21:15 YESU alikuwa anataka kumuondolea ule moyo wa kumkana YESU mara3.

1SAMWEL3: NENA BWANA KWA KUWA MTUMISHI WAKO ANASIKIA, huu ni moyo wa unyenyekevu. Unakupa kuisikia sauti ya MUNGU pia kuijua hiyo sauti ya MCHUNGAJI MMOJA.
Mlango wa kupokea huo moyo; Ni kukubali kufundishika usifikiri MUNGU atashuka na suti na miwani.
Siri ya uzuri kwa mabinti ni kuwa na moyo wa unyenyekevu na toba, na akili nzuri unaipata kwa unyenyekevu na toba. RAIS amesema kwa kila jambo mtangulize kwanza MUNGU huu ni unyenyekevu.
Usitake kuchangia pointi kila unachokisikia , acha kusukumia wengine makosa . Wakili amesema; “am talking my life”.
Hata kama kichwa wako hakupendi ondoka na moyo wa unyenyekevu leo lazima atakuambia anakupenda. Majira hii unapokwama muite WAKILI WA MUNGUUUU!!!! Aibu yako itafutika mara moja.
MUNGU HAKOSEI, WAKILI HAKOSEI alichokubali WAKILI na MUNGU amekikubali. Alichokikataa WAKILI na MUNGU amekikataa, aliyekubaliwa na WAKILI na MUNGU amemkubali.
KILA MMOJA ATAMBUE KUWA MOYO WA UNYENYEKEVU NI WEWE UKUBALI KUCHUNGWA NA MCHUNGAJI MMOJA PEKEE zaburi23.

Jumamosi, 21 Januari 2017


MAJIRA NA NYAKATI YA MOYO MMOJA HALISI KWA KILA MWENYE HAKI NDANI YA UUMBAJI WOTE

Wakili wa MUNGU alianza kwa shukrani kwa kuwa moyo wa pili hauta onekana kwa yule atendae kwa haki. Moyo wa kufa, kaburi n.k hautakuwepo tena.
“Nimejifunza kuwa, kusudi la MUNGU halizuiliwi hata kama walikuona hufai n.k
watakutafuta tu.
Hakuna atakae kumbuka jinsi ulivyopakwa mavi n.k au jinsi walivyotukana Siloamu.”
Shukrani kwa MUNGU kwa moyo ninaoondoka nao ni Moyo wa MUNGU.
Aidha Wakili wa MUNGU leo amefundisha kwa kufafanua mistari miwili tu ya NENO ambayo ni Matendo3:19,21 akaifunua kuwa matendo3:19 (mtaji) na 21 (faida).
Kwa moyo moja utakao ondoka nayo leo baada ya toba hata kama ulikuwa tambala la deki hutakuwa hivyo ni lazima watakutafuta.
Maana unaondoka na madhabahu ya moyo mpya na kila kitu kinafunuliwa kwa upya ikiwa ni pamoja na kiungo kimoja kimoja pia kinafunuliwa kwa upya.
Wakili wa MUNGU aliongoza wenye haki kutoa sadaka maalumu ya madhabahu ya kupokea moyo mpya na kila kitu kufunuliwa kwa upya kutokana na majira na nyakati ya moyo mmoja halisi kwa kila mwenye haki ndani ya uumbaji wote.
Toba kwa ajili ya uliofanyiwa bila kujua katika haya fuatayo:-
#kuwaza,
#kunena,
#kutenda,
#kushitaki
  #na kuomba kinyume.
Toba kwaajili ya uliyofanya wewe mwenyewe bila kujua au kwa kujua;-
#kuwaza
#kunena
#kutenda
#kushtaki
#kuomba.
Yawezekana ulipokuwa tumboni kuna waliokuwazia vibaya vikaingia mpaka kwenye damu na hata leo bado tunaviona, futa kwa Damu ya MUNGU.
Kuna waliokuwazia mabaya tangu tumboni mwa mama yako eg. Atazaa malaya, jambazi hata leo unaonekana hivyo.
Hata ulipokuja Siloamu siku ya kwanza ukaongozwa sara ya toba kuna waliokuwazia vibaya, kuzungukwa zungukwa kwa ayaliyowazwa.
Kuna yaliyonenwa yaliyomabaya unayoyajua na usiyoyajua leo tutubu.
Kila kitu kitakuwa kipya baada ya toba hii.
Like Father
        Like Son.
Kuna uliyotendewa na wengine umejitahidi kusahau lakini bado unakumbuka.
Kuna mambo ulishtakiwa hata pasipo wewe kujua tutubu.
Kuna mengi umeombewa kinyume mengine unajua na mengine hujui tutubu kwa hayo yote.
Kuna uliyowahi kufanya wewe mwenyewe kwa sababu ya uliyofanyiwa, kuwaza kinyume na MUNGU, Kristo, Kanisa, Wakili wa MUNGU, Taifa.
Kuna uliyowaza tofauti na kinyume na MUNGU ukasema wana kijicho leo tutubu.
Kuna niliyoyanena kinyume ukifikiri uko sahihi kumbe haupo sahihi.
MUNGU akupe Neema ya kushinda kujihesabia haki kwa kutubu kwa yale yote tuliyotenda kinyume kwa sababu ya yale niliyonena.
Daniel na Nehemia walitubu kwaajili ya ambayo hawakukosa taifa likapona.
Kuna uliyowahi kushitaki, kujishtaki. Kufuta kwa toba niliyoomba kinyume na wengine.
TUbu kwaajili ya kuendelea kuishi ktk majira ya 1-6 leo MUNGU atusamehe.
Kama ukimaanisha leo unatoka na vitu vizuri ambavyo havijakuonekana kwani haya ndio yalikamatia kizazi cha kwanza hadi cha nne.
Isaya 30:20 MUNGU leo ameyang’oa yote mabaya.
Haya yote yalikuwa yanasababisa kukosa kuanzia kizazi cha kwanza hadi cha nne, kung’ang’ania majira ya kwanza hadi ya sita.
“haya ndio yaliokuwa yakisabababisha mnifananishe na waliotumwa. Mimi sio nabii, ,mchungaji n.k, nimembeba MUNGU   Aliyetuma wote.
Ukiniona imetosha hata usiponishika mkono”
Kwa sadaka hii kila mmoja akafute kisasi cha ushindi na kishindo cha ushindi.
Moyo wa uzalishaji: Mathayo 12:33
Leo tumepokea moyo wa uzalishaji kila utakacho shika kitapendwa na kile utakacho tamka kita tokea.
Huo ndio moyo wa uzalishaji, utakwenda mahali kuliko kauka kuta badilika saa hiyo hiyo.
Kila mmoja ata tamani uendeshe gari lake ili kiwanda chake kiende juu. Wewe subiri tu magari yanakuja.
Kwa majira ya leo ukienda sehemu ya jangwa ndani ya mwezi mmoja lazima:-
*watajua kupika maandazi.
*watakula matunda.
*watajua kuuza matunda.
*wakifundishwa wanaelewa.
Moyo wa uzalishaji unakupa kujua au kupokea kila kitu kizuri.
Moyo huo unasababisha wengine kufahamu walivyokuwa hawafahamu kwa mwezi mmoja. Wote wenye viwanda watatamani utumie bidhaa zao. 
“Leo umeondoka na moyo wa uzalishaji”
Aidha alihitimisha ibada hiyo kwa kusimamisha moto ulao kwa yeyote aliyekuwa amejipanga kuiba ushindi wa kizazi cha MUNGU wa leo!

Ijumaa, 20 Januari 2017


THAMANI NA FAIDA YA KUNG’OA KIINI CHA UOVU NDANI YA UUMBAJI WOTE


Wakili wa MUNGU alianza kwa kuunganisha na msingi wa ibada ambapo Mtendaji wa Wakili wa MUNGU leo amefuta viapo alivyowahi kuweka kwa waliotumwa na kuKiweka leo kwa Mungu Aliyetuma wote.
Wakili wa MUNGU alisema kuwa, “ jengo lilisubiri kiapo hiki kwa muda mrefu, sasa tuna hakika ya safari”.
Mtendaji wa Wakili Wa MUNGU alisimamisha Kiapo kuwa: *“Niko Hai na sintakufa;*
*MUNGU hata-aibika*
*Kristo hata-aibika*
*Wakili Wa MUNGU hata-aibika*
*Kanisa halita-aibika*
*Kizazi hakita-aibika*
*Taifa halita-aibika*
Wakili alisema Kiapo hiki kimekata kata mabomba yote machafu.
Aidha Wakili wa MUNGU aliongoza wenye haki kutoa sadaka maalum ya Mith 4:23 kwamba Moyo wako hautachakaa maana unalindwa na kiapo, una ulinzi usiokuwa wa kawaida na una uhakika usiokuwa wa kawaida.
Moyo wako hautaingiwa na mshale wowote, kila kitu kita leta faida.
Sadaka hii ina simamisha agano kuwa hutafadhaika tena kwa lolote.
*“Sasa rasmi ufalme wa MUNGU umehama kutoka mashariki ya kati kuja hapa, hakuna siku kama ya leo. Hutafadhaika tena, umbaji umetaharuki.”* aliongeza Wakili katikati ya shukrani.
MUNGU aliwahi kufadhaishwa na *kerubi
   *Adamu
   *mwanamke
   *kizazi cha 1-4
   *waliotumwa
   *kanisa la kizazi 1-4
   *Leo ni mwisho.
"Nasimamisha uhalisi wa kanisa kutofadhaishwa na yeyote"
Je ni ipi thamani na faida ya kungoa kiini cha uovu ndani ya umbaji wote?
Utakaa juu tu, hutashuka hata siku moja. isaya 66:22. MUNGU Hayuko chini, yuko juu tu. Hata akikaa ndani ya moyo Anakaa ndani ya moyo ulio juu.
Sasa hakuna chochote kitakacho kushusha chini tena. Wote waliomwasi MUNGU watakuwa mizoga na watu wote wataokoka.
“ MUNGU Anakaa katikati ya wanadamu yaani juu ya nchi na wote watamabudu na kwa Yule anaemwamini anakuwa kuhani wake na kristo.
MUNGU Anabadilisha mtazamo uliokuwa nao kuhusu YEYE. Ile MUNGU Ameleta mbingu mpya  na nchi mpya.”
Kwa nini Mungu amebadili mtazamo?
Wote waliotumwa walikuwa Mungu, lakini mambo haya kwenda vizuri. Sasa MUNGU Hawezi kuendelea na utaratibu uliopita.
Hekima ya kizazi cha 1-4 Leo umefutwa, utendaji wa kizazi cha 1-4 ni mwisho umefutwa Leo. Isaya66:22 na Ufunuo21:1-3 tazama ya kale yote yamepita sasa yamekuwa mapya.
Hekima ya MUNGU sasa ni ktk viwango vya mstari ulionyooka nyuzi 180, hakuna DOA, hakuna kukosea, hakuna kujitetea, hakuna kujihesabia HAKI yaani ukubali kumilikiwa na MUNGU.
“Alisema kila goti ni lazima lipige mbele zake, jambo hilo ni sasa hivi. MUNGU Akiendelea na utendaji wa zamani, dunia haitatikisika na watu hawatakuja na YEYE Anataka waje.”
Hekima ya MUNGU kuwa ndani ya kila mmoja. Yeremia 31:34
MUNGU kuharibu hekima zilizokuwepo, itabaki hekima ya MUNGU peke yake isiyo na doa. Hekima ya MUNGU ni mstari ulionyooka.
Mlima wa uzalishaji umerudi madhabahuni. Mlima wa uzalishaji ulikuwa bado duniani lakini sasa imerejea kanisani.
Makuhani wa madhabahuni walipotumwa nje walikuwa wakitafuta kuongeza watu sio uzalishaji kwa kuwa mlima wa uzalishaji ulikuwa duniani. Sasa hivi makuhani watafuatilia kwa kila mmoja kuona wanacho zalisha na kukiinua.
Maana tuna nguvu ya uzao, kustawi na kuongezeka.
2 falme 2:19 sasa hivi takataka zote zimerudi kwa waliomwasi MUNGU. Nguvu ya uzao na kuongezeka sasa imerejea,
“MUNGU Amefuta kabisa ule mwanzo  wa uharibifu, Mwanzo Malidadi upo hapa Gosheni (Tanzania). Mwambie kila mmoja hilo.
Sasa shamba la MUNGU limerudi kanisani, waovu walikuwa wamegawana maploti. Leo MUNGU Amekurejeshea ploti kila unachofaya kina tiki.”
“Umeingia mahali pako na mbegu ya kupanda unayo, ukipanda itaota na utavuna. Uta barikiwa na kumiliki mlango wa adui zako. Kichwa wako Amerejea na nguvu za ajabu Ana maploti ya kutisha yenye kila unacho kihitaji.”
Ile bustani ya Eden ilitakiwa kuwa Gosheni sasa imerejea maana waligawana gawana sana, ni lazima waje kuwekeza hapa maana kuna connection ya uzalishaji wa rohoni. Maana mmiliki Amekuja Mwenyewe, Mwenye shamba Amekuja wapangaji wote Amewatoa.
Waliomwasi MUNGU ndio basi tena, na waliokuwa wakiku dharau wata kushang’aa.
“sadaka ya leo ilikuwa inakuanda kuchukua ploti kama utachukua ploti ya  kiwanda  cha uzalishaji au makampuni, masupermarket n.k na ulinzi moja halisi unao.
Nimekupa homework kesho uniambie ni ploti ipi unachukua kwenye shamba hilo.”
Karamu:- sheria ya roho wa uzima, leo inakupa, mlima wa uzalishaji na ikupe ufahamu ya kuchukua ploti yako kwenye shamba la MUNGU.

Alhamisi, 19 Januari 2017


BAADA YA KIAPO NI AGANO

Wakili Wa MUNGU alianza  kwa shukrani kwa kusanyiko kubwa lenye Moyo Mmoja Wa MUNGU, MUNGU amepata kusanyiko kubwa sana kizazi hiki lenye Moyo mmoja Wa MUNGU.
Ambapo pia tumepakwa mafuta ya ukamilifu na utimilifu.
Aidha Wakili wa MUNGU ameongoza wenye haki kutoa Sadaka Maalumu ya kuondoa kabisa kiini cha uovu kilichokuwa kinakuletea shida kwenye familia, Agano lako, biashara, kampuni, mashamba, viwanda, nk ndani ya Moyo wako.
Yer  50:20 Maovu yamefutwa. Dhambi, uovu na uasi utatafutwa wala hautaonekana.
Ebr 8:10-12 Maovu yamefutwa, haya-kumbukwi tena
Isa 30:20-21 Sauti ya MUNGU inasikika ikisema  “NJIA NI HII HAPA”
Huyu ndiye huyu siye.
Kila Maovu, dhambi na uasi kwa Sadaka hiyo aliigeuza kuwa Sadaka ya Shukrani  ili MUNGU kutenda zaidi ya tuliyo-shukuru.
Kuna mwingine amekuwa akijitahidi kuachana na uongo, rushwa, kufyonza n.k leo kiini hicho kinang’oka, Kiini cha kupenda udaku na mambo ya dunia kinang’oka, Kiini cha kusengenya wengine n.k kinang’oka.
Shukrani kwa MUNGU kwa kuwa mwenye Haki  amefika mahali MUNGU anapoishi mahali pa Moyo mmoja Halisi.
Moyo ni chanzo cha kila kitu, sasa tuna-Moyo wa MUNGU.
“Acha Moyo wako ufurahi, furaha yako inapiga maadui. Leo ni siku ya ajabu ufurahi”
Chujio la MUNGU Kristo na Wakili wako Kanisa lipo kazini. Nakusema kiini cha moyo ni level ya juu mno.
MUNGU anaondoa kiini cha wewe kukusudia mema yakatokea mabaya, kuanza vizuri na kumaliza vibaya anang’oa.
Kukusudia kanisa anatokea mwanamke, kukusudia kichwa anatkea mwanaume anang’oa.
MUNGU Kung’oa kiini cha:
Kuanza vizuri kuishia vibaya
Wazo la kwanza na la pili
Utasa, kuachana, mafarakano n.k
Dini na dhehebu, Mti wa ujuzi wa mema na mabaya Ajali, kifo na mauti, wachawi, wanga, wanajimu, washirikina, magonjwa yote MUNGU anang’oa.
Uzee, magonjwa
Nafsi yako kuibiwa
Kulima ukapanda mbegu njema palepale madumadu, tunutu, wakaingia shambani kula mazao leo ni mwisho.
Kiini cha kukuta kaskazini matajiri kusini ni masikini kinafutwa.
Mwanzo wa uharibifu kiini chake kimeng’olewa kimeondolewa.
“Kiapo chochote kina-Agano. Katika kila kiapo ulichoapa kina-agano ndani yake, Kuna viapo ulivyoapa kwa kujua/kutokujua na ndotoni sasa ndani ya kiapo hicho kuna-Agano.
Ili tuweze kukaa na huyu ni lazima tuingie Agano na MUNGU.
Katika Mwa 22:15 MUNGU alimwapia Ibrahimu akatengeneza Agano, Agano ni lazima liwe na Sadaka.
“Wakili Wa MUNGU ameapa na sisi tuna-Agano la kuto-aibika lakini ni kwa Yule atendae kwa haki tu, kwa mwovu haitokei. Wewe umemfuata MUNGU Wa kweli huta-aibika Milele”
Amesema kuna viapo unaweza kuapa bila wewe mwenyewe kujua, pia katika kila kiapo unachofuta unatakiwa ufute na Agano uliloweka.
Aidha amesisitiza kila mmoja kufuta maagano yote ili yasije kuwa mtego kwako mwenye haki.
Leo futa viapo hivyo ili uwe huru na MUNGU awe kuachilia ule utajiri halisi pale ulipo, unapomuapia MUNGU naye anakuapia na wewe.
Leo Kanisa tunamuapia MUNGU kwamba hatutamuacha milele.
Warumi 9:4 MUNGU aliwaapia kwa viapo hivyo na maagano ya MUNGU kuwa nasi.
“Kiapo kimesimama na Agano limesimama usiwe na wasiwasi”